104. Al-Humazah - Qurani
- 1. Ole wake kila safihi, msengenyaji!
- 2. Aliye kusanya mali na kuyahisabu.
- 3. Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele!
- 4. Hasha! Atavurumishwa katika H`ut`ama.
- 5. Na nani atakujuvya ni nini H`ut`ama?
- 6. Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa.
- 7. Ambao unapanda nyoyoni.
- 8. Hakika huo utafungiwa nao
- 9. Kwenye nguzo zilio nyooshwa.