Al-Muddaththir - QURAN - Harun Yahya
-
1. Ewe uliye jigubika!
-
2. Simama uonye!
-
3. Na Mola wako Mlezi mtukuze!
-
4. Na nguo zako, zisafishe.
-
5. Na yaliyo machafu yahame!
-
6. Wala usitoe kwa kutaraji kuzidishiwa.
-
7. Na kwa ajili ya Mola wako Mlezi, subiri!
-
8. Basi litapo pulizwa barugumu,
-
9. Siku hiyo, basi, itakuwa siku ngumu.
-
10. Kwa makafiri haitakuwa nyepesi.
-
11. Niache peke yangu na niliye muumba;
-
12. Na nikamjaalia awe na mali mengi,
-
13. Na wana wanao onekana,
-
14. Na nikamtgenezea mambo vizuri kabisa.
-
15. Kisha anatumai nimzidishie!
-
16. Hasha! Kwani hakika yeye alikuwa akizifanyia inadi Aya zetu!
-
17. Nitamtesa kwa mateso yasio wezekana.
-
18. Kwani hakika yeye alifikiri na akapima.
-
19. Basi ameangamia! Vipi alivyo pima!
-
20. Tena ameangamia! Vipi alivyo pima!
-
21. Kisha akatazama,
-
22. Kisha akakunja kipaji, na akanuna.
-
23. Kisha akaipa kisogo haki, na akatakabari.
-
24. Na akasema: Haya si chochote ila ni uchawi ulio nukuliwa.
-
25. Haya si chochote ila kauli ya binaadamu.
-
26. Nitakuja mtia kwenye Moto wa Saqar.
-
27. Na nini kitakujuulisha ni nini huo Moto wa Saqar?
-
28. Haubakishi wala hausazi.
-
29. Unababua ngozi iwe nyeusi.
-
30. Juu yake wapo kumi na tisa.
-
31. Na hatukuwafanya walinzi wa Motoni ila ni Malaika, wala hatukuifanya idadi yao hiyo ila kuwatatanisha walio kufuru, wapate kuwa na yakini walio pewa Kitabu, na wazidi Imani wale walio amini, wala wasiwe na shaka walio pewa Kitabu na Waumini, na wapate kusema wenye maradhi katika nyoyo zao na makafiri: Mwenyezi Mungu amekusudia nini kwa mfano huu? Ndio kama hivyo Mwenyezi Mungu humwacha apotee amtakaye, na humwongoa amtakaye. Na hapana yeyote anaye jua majeshi ya Mola wako Mlezi ila Yeye tu. Na haya si chochote ila ni ukumbusho kwa binaadamu.
-
32. Hasha! Naapa kwa mwezi!
-
33. Na kwa usiku unapo kucha!
-
34. Na kwa asubuhi inapo pambazuka!
-
35. Hakika huo Moto ni katika mambo yaliyo makubwa kabisa!
-
36. Ni onyo kwa binaadamu,
-
37. Kwa anaye taka miongoni mwenu kutangulia au kuchelewa.
-
38. Kila nafsi imo rahanini kwa mabaya iliyo yachuma.
-
39. Isipo kuwa watu wa kuliani.
-
40. Hao watakuwa katika Mabustani, wawe wanaulizana
-
41. Khabari za wakosefu:
-
42. Ni nini kilicho kupelekeni Motoni?
-
43. Waseme: Hatukuwa miongoni walio kuwa wakisali.
-
44. Wala hatukuwa tukiwalisha masikini.
-
45. Na tulikuwa tukizama pamoja na walio zama katika maovu.
-
46. Na tulikuwa tukiikanusha siku ya malipo.
-
47. Mpaka yakini ilipo tufikia.
-
48. Basi hautawafaa kitu uombezi wa waombezi.
-
49. Basi wana nini hata wanapuuza onyo hili?
-
50. Kama kwamba wao ni mapunda walio timuliwa,
-
51. Wanao mkimbia simba!
-
52. Ati kila mmoja katika wao anataka apewe nyaraka zilizo funuliwa.
-
53. Hasha! Kwani wao hawaiogopi Akhera?
-
54. Hasha! Kwa hakika huu ni ukumbusho!
-
55. Basi anaye taka atakumbuka.
-
56. Na hawatakumbuka isipo kuwa Mwenyezi Mungu atake. Uchamngu ni kwake Yeye, na msamaha ni wake Yeye.
SHIRIKI
1
Al-Fatihah
2
Al Baqara
3
Ali `Imran
4
An-Nisa
5
Al-Ma`idah
6
Al-An`am
7
Al-A`raf
8
Al-Anfal
9
At-Tawbah
10
Yunus
11
Hud
12
Yusuf
13
Ar-Ra`d
14
Ibrahim
15
Al-Hijr
16
An-Nahl
17
Al-Isra
18
Al-Kahf
19
Maryam
20
Taha
21
Al-Anbya
22
Al-Haj
23
Al-Mu`minun
24
An-Nur
25
Al-Furqan
26
Ash-Shu`ara
27
An-Naml
28
Al-Qasas
29
Al-`Ankabut
30
Ar-Rum
31
Luqman
32
As-Sajdah
33
Al-Ahzab
34
Saba
35
Faatir
36
Ya-Sin
37
As-Saffat
38
Sad
39
Az-Zumar
40
Ghafir
41
Fussilat
42
sh-Shuraa
43
Az-Zukhruf
44
Ad-Dukhan
45
Al-Jathiyah
46
Al-Ahqaf
47
Muhammad
48
Al-Fath
49
Al-Hujurat
50
Qaf
51
Adh-Dhariyat
52
At-Tur
53
An-Najm
54
Al-Qamar
55
Ar-Rahman
56
Al-Waqi`ah
57
Al-Hadid
58
Al-Mujadila
59
Al-Hashr
60
Al-Mumtahanah
61
As-Saf
62
Al-Jumu`ah
63
Al-Munafiqun
64
At-Taghabun
65
At-Talaq
66
At-Tahrim
67
Al-Mulk
68
Al-Qalam
69
Al-Haqqah
70
Al-Ma`arij
71
Nuh
72
Al-Jinn
73
Al-Muzzammil
74
Al-Muddaththir
75
Al-Qiyamah
76
Al-Insan
77
Al-Mursalat
78
An-Naba
79
An-Nazi`at
80
Abasa
81
At-Takwir
82
Al-Infitar
83
Al-Mutaffifin
84
Al-Inshiqaq
85
Al-Buruj
86
At-Tariq
87
Al-A`la
88
Al-Ghashiyah
89
Al-Fajr
90
Al-Balad
91
Ash-Shams
92
Al-Layl
93
Ad-Duhaa
94
Ash-Sharh
95
At-Tin
96
Al-`Alaq
97
Al-Qadr
98
Al-Bayyinah
99
Az-Zalzalah
100
Al-`Adiyat
101
Al-Qari`ah
102
At-Takathur
103
Al-`Asr
104
Al-Humazah
105
Al-Fil
106
Quraysh
107
Al-Ma`un
108
Al-Kawthar
109
Al-Kafirun
110
An-Nasr
111
Al-Masad
112
Al-Ikhlas
113
Al-Falaq
114
An-Nas