An-Nazi`at - QURAN - Harun Yahya
-
1. Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu,
-
2. Na kwa wanao toa kwa upole,
-
3. Na wanao ogelea,
-
4. Wakishindana mbio,
-
5. Wakidabiri mambo.
-
6. Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka,
-
7. Kifuate cha kufuatia.
-
8. Siku hiyo nyoyo zitapiga piga,
-
9. Macho yatainama chini.
-
10. Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?
-
11. Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?
-
12. Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!
-
13. Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,
-
14. Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!
-
15. Je! Imekufikia hadithi ya Musa?
-
16. Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T`uwaa, akamwambia:
-
17. Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri.
-
18. Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?
-
19. Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.
-
20. Basi alimwonyesha Ishara kubwa.
-
21. Lakini aliikadhibisha na akaasi.
-
22. Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.
-
23. Akakusanya watu akanadi.
-
24. Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.
-
25. Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.
-
26. Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa.
-
27. Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!
-
28. Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.
-
29. Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake.
-
30. Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.
-
31. Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake,
-
32. Na milima akaisimamisha,
-
33. Kwa nafuu yenu na mifugo yenu.
-
34. Basi itakapo fika hiyo balaa kubwa,
-
35. Siku ambayo mtu atakumbuka aliyo yafanya,
-
36. Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona,
-
37. Basi ama yule aliye zidi ujeuri,
-
38. Na akakhiari maisha ya dunia,
-
39. Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!
-
40. Na ama yule anaye ogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio,
-
41. Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!
-
42. Wanakuuliza Saa (ya Kiyama) itakuwa lini?
-
43. Una nini wewe hata uitaje?
-
44. Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake.
-
45. Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuikhofu.
-
46. Ni kama kwamba wao siku watapo iona (hiyo Saa) hawakukaa ila jioni moja tu, au mchana wake.
SHIRIKI
1
Al-Fatihah
2
Al Baqara
3
Ali `Imran
4
An-Nisa
5
Al-Ma`idah
6
Al-An`am
7
Al-A`raf
8
Al-Anfal
9
At-Tawbah
10
Yunus
11
Hud
12
Yusuf
13
Ar-Ra`d
14
Ibrahim
15
Al-Hijr
16
An-Nahl
17
Al-Isra
18
Al-Kahf
19
Maryam
20
Taha
21
Al-Anbya
22
Al-Haj
23
Al-Mu`minun
24
An-Nur
25
Al-Furqan
26
Ash-Shu`ara
27
An-Naml
28
Al-Qasas
29
Al-`Ankabut
30
Ar-Rum
31
Luqman
32
As-Sajdah
33
Al-Ahzab
34
Saba
35
Faatir
36
Ya-Sin
37
As-Saffat
38
Sad
39
Az-Zumar
40
Ghafir
41
Fussilat
42
sh-Shuraa
43
Az-Zukhruf
44
Ad-Dukhan
45
Al-Jathiyah
46
Al-Ahqaf
47
Muhammad
48
Al-Fath
49
Al-Hujurat
50
Qaf
51
Adh-Dhariyat
52
At-Tur
53
An-Najm
54
Al-Qamar
55
Ar-Rahman
56
Al-Waqi`ah
57
Al-Hadid
58
Al-Mujadila
59
Al-Hashr
60
Al-Mumtahanah
61
As-Saf
62
Al-Jumu`ah
63
Al-Munafiqun
64
At-Taghabun
65
At-Talaq
66
At-Tahrim
67
Al-Mulk
68
Al-Qalam
69
Al-Haqqah
70
Al-Ma`arij
71
Nuh
72
Al-Jinn
73
Al-Muzzammil
74
Al-Muddaththir
75
Al-Qiyamah
76
Al-Insan
77
Al-Mursalat
78
An-Naba
79
An-Nazi`at
80
Abasa
81
At-Takwir
82
Al-Infitar
83
Al-Mutaffifin
84
Al-Inshiqaq
85
Al-Buruj
86
At-Tariq
87
Al-A`la
88
Al-Ghashiyah
89
Al-Fajr
90
Al-Balad
91
Ash-Shams
92
Al-Layl
93
Ad-Duhaa
94
Ash-Sharh
95
At-Tin
96
Al-`Alaq
97
Al-Qadr
98
Al-Bayyinah
99
Az-Zalzalah
100
Al-`Adiyat
101
Al-Qari`ah
102
At-Takathur
103
Al-`Asr
104
Al-Humazah
105
Al-Fil
106
Quraysh
107
Al-Ma`un
108
Al-Kawthar
109
Al-Kafirun
110
An-Nasr
111
Al-Masad
112
Al-Ikhlas
113
Al-Falaq
114
An-Nas