Al-Qalam - QURAN - Harun Yahya
-
1. Nuun. Naapa kwa kalamu na yale wayaandikayo,
-
2. Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.
-
3. Na kwa hakika wewe una malipo yasiyo katika.
-
4. Na hakika wewe una tabia tukufu.
-
5. Karibu utaona, na wao wataona,
-
6. Ni nani kati yenu aliye pandwa na wazimu.
-
7. Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliye ipotea Njia yake, na Yeye ndiye anaye wajua zaidi walio ongoka.
-
8. Basi usiwat`ii wanao kadhibisha.
-
9. Wanatamani lau unge lainisha ili nao wakulainishie.
-
10. Wala usimt`ii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa,
-
11. Mtapitapi, apitaye akifitini,
-
12. Mwenye kuzuia kheri, dhaalimu, mwingi wa madhambi,
-
13. Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu.
-
14. Ati kwa kuwa ana mali na watoto!
-
15. Anapo somewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uwongo za watu wa zamani!
-
16. Tutamtia kovu juu ya pua yake.
-
17. Hakika tumewajaribu hawa kama tulivyo wajaribu wale wenye shamba, walipo apa kwamba watayavuna mazao yake itakapo kuwa asubuhi.
-
18. Wala hawakusema: Mungu akipenda!
-
19. Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!
-
20. Likawa kama usiku wa giza.
-
21. Asubuhi wakaitana.
-
22. Ya kwamba nendeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.
-
23. Basi walikwenda na huku wakinong`onezana,
-
24. Ya kuwa leo hata masikini mmoja asikuingilieni.
-
25. Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.
-
26. Basi walipo liona, wakasema: Hakika tumepotea!
-
27. Bali tumenyimwa!
-
28. Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?
-
29. Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.
-
30. Basi wakakabiliana kulaumiana wao kwa wao.
-
31. Wakasema: Ole wetu! Tulikuwa tumeikiuka mipaka!
-
32. Asaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
-
33. Namna hivi yanakuwa mateso, na bila ya shaka mateso ya Akhera ni makubwa zaidi, laiti wangeli jua!
-
34. Hakika wachamngu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi.
-
35. Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu?
-
36. Mna nini? Mnahukumu vipi?
-
37. Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?
-
38. Kuwa mtapata humo mnayo yapenda?
-
39. Au mnazo ahadi za viapo juu yetu za kufika Siku ya Kiyama ya kuwa hakika mtapata kila mnayo jihukumia?
-
40. Waulize: Ni nani miongoni mwao dhamini wa haya?
-
41. Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli.
-
42. Siku utakapo wekwa wazi mundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza,
-
43. Macho yao yatainama chini, fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipo kuwa wazima -
-
44. Basi niache na wanao kadhibisha maneno haya! Tutawavutia kidogo kidogo kwa mahali wasipo pajua.
-
45. Na ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara.
-
46. Au unawaomba ujira, na wao wanaemewa na gharama hiyo?
-
47. Au iko kwao siri, basi wao wanaiandika?
-
48. Basi ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi, wala usiwe kama mmezwa na samaki, alipo nadi naye kazongwa.
-
49. Kama isingeli mfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angeli tupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.
-
50. Lakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.
-
51. Na walio kufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanapo sikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.
-
52. Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
SHIRIKI
1
Al-Fatihah
2
Al Baqara
3
Ali `Imran
4
An-Nisa
5
Al-Ma`idah
6
Al-An`am
7
Al-A`raf
8
Al-Anfal
9
At-Tawbah
10
Yunus
11
Hud
12
Yusuf
13
Ar-Ra`d
14
Ibrahim
15
Al-Hijr
16
An-Nahl
17
Al-Isra
18
Al-Kahf
19
Maryam
20
Taha
21
Al-Anbya
22
Al-Haj
23
Al-Mu`minun
24
An-Nur
25
Al-Furqan
26
Ash-Shu`ara
27
An-Naml
28
Al-Qasas
29
Al-`Ankabut
30
Ar-Rum
31
Luqman
32
As-Sajdah
33
Al-Ahzab
34
Saba
35
Faatir
36
Ya-Sin
37
As-Saffat
38
Sad
39
Az-Zumar
40
Ghafir
41
Fussilat
42
sh-Shuraa
43
Az-Zukhruf
44
Ad-Dukhan
45
Al-Jathiyah
46
Al-Ahqaf
47
Muhammad
48
Al-Fath
49
Al-Hujurat
50
Qaf
51
Adh-Dhariyat
52
At-Tur
53
An-Najm
54
Al-Qamar
55
Ar-Rahman
56
Al-Waqi`ah
57
Al-Hadid
58
Al-Mujadila
59
Al-Hashr
60
Al-Mumtahanah
61
As-Saf
62
Al-Jumu`ah
63
Al-Munafiqun
64
At-Taghabun
65
At-Talaq
66
At-Tahrim
67
Al-Mulk
68
Al-Qalam
69
Al-Haqqah
70
Al-Ma`arij
71
Nuh
72
Al-Jinn
73
Al-Muzzammil
74
Al-Muddaththir
75
Al-Qiyamah
76
Al-Insan
77
Al-Mursalat
78
An-Naba
79
An-Nazi`at
80
Abasa
81
At-Takwir
82
Al-Infitar
83
Al-Mutaffifin
84
Al-Inshiqaq
85
Al-Buruj
86
At-Tariq
87
Al-A`la
88
Al-Ghashiyah
89
Al-Fajr
90
Al-Balad
91
Ash-Shams
92
Al-Layl
93
Ad-Duhaa
94
Ash-Sharh
95
At-Tin
96
Al-`Alaq
97
Al-Qadr
98
Al-Bayyinah
99
Az-Zalzalah
100
Al-`Adiyat
101
Al-Qari`ah
102
At-Takathur
103
Al-`Asr
104
Al-Humazah
105
Al-Fil
106
Quraysh
107
Al-Ma`un
108
Al-Kawthar
109
Al-Kafirun
110
An-Nasr
111
Al-Masad
112
Al-Ikhlas
113
Al-Falaq
114
An-Nas