logo HARUN YAHYA

Al-Qalam - QURAN - Harun Yahya

  • 1. Nuun. Naapa kwa kalamu na yale wayaandikayo,
  • 2. Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.
  • 3. Na kwa hakika wewe una malipo yasiyo katika.
  • 4. Na hakika wewe una tabia tukufu.
  • 5. Karibu utaona, na wao wataona,
  • 6. Ni nani kati yenu aliye pandwa na wazimu.
  • 7. Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliye ipotea Njia yake, na Yeye ndiye anaye wajua zaidi walio ongoka.
  • 8. Basi usiwat`ii wanao kadhibisha.
  • 9. Wanatamani lau unge lainisha ili nao wakulainishie.
  • 10. Wala usimt`ii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa,
  • 11. Mtapitapi, apitaye akifitini,
  • 12. Mwenye kuzuia kheri, dhaalimu, mwingi wa madhambi,
  • 13. Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu.
  • 14. Ati kwa kuwa ana mali na watoto!
  • 15. Anapo somewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uwongo za watu wa zamani!
  • 16. Tutamtia kovu juu ya pua yake.
  • 17. Hakika tumewajaribu hawa kama tulivyo wajaribu wale wenye shamba, walipo apa kwamba watayavuna mazao yake itakapo kuwa asubuhi.
  • 18. Wala hawakusema: Mungu akipenda!
  • 19. Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!
  • 20. Likawa kama usiku wa giza.
  • 21. Asubuhi wakaitana.
  • 22. Ya kwamba nendeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.
  • 23. Basi walikwenda na huku wakinong`onezana,
  • 24. Ya kuwa leo hata masikini mmoja asikuingilieni.
  • 25. Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.
  • 26. Basi walipo liona, wakasema: Hakika tumepotea!
  • 27. Bali tumenyimwa!
  • 28. Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?
  • 29. Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.
  • 30. Basi wakakabiliana kulaumiana wao kwa wao.
  • 31. Wakasema: Ole wetu! Tulikuwa tumeikiuka mipaka!
  • 32. Asaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
  • 33. Namna hivi yanakuwa mateso, na bila ya shaka mateso ya Akhera ni makubwa zaidi, laiti wangeli jua!
  • 34. Hakika wachamngu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi.
  • 35. Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu?
  • 36. Mna nini? Mnahukumu vipi?
  • 37. Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?
  • 38. Kuwa mtapata humo mnayo yapenda?
  • 39. Au mnazo ahadi za viapo juu yetu za kufika Siku ya Kiyama ya kuwa hakika mtapata kila mnayo jihukumia?
  • 40. Waulize: Ni nani miongoni mwao dhamini wa haya?
  • 41. Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli.
  • 42. Siku utakapo wekwa wazi mundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza,
  • 43. Macho yao yatainama chini, fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipo kuwa wazima -
  • 44. Basi niache na wanao kadhibisha maneno haya! Tutawavutia kidogo kidogo kwa mahali wasipo pajua.
  • 45. Na ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara.
  • 46. Au unawaomba ujira, na wao wanaemewa na gharama hiyo?
  • 47. Au iko kwao siri, basi wao wanaiandika?
  • 48. Basi ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi, wala usiwe kama mmezwa na samaki, alipo nadi naye kazongwa.
  • 49. Kama isingeli mfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angeli tupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.
  • 50. Lakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.
  • 51. Na walio kufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanapo sikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.
  • 52. Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
SHIRIKI
Facebook
X
WhatsApp
Telegram
QR Code
QR Code