Adh-Dhariyat - QURAN - Harun Yahya
-
1. Naapa kwa pepo zinazo tawanya,
-
2. Na zinazo beba mizigo,
-
3. Na zinazo kwenda kwa wepesi.
-
4. Na zinazo gawanya kwa amri,
-
5. Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka ni kweli,
-
6. Na kwa hakika malipo bila ya shaka yatatokea.
-
7. Naapa kwa mbingu zenye njia,
-
8. Hakika nyinyi bila ya shaka mmo katika kauli inayo khitalifiana.
-
9. Anageuzwa kutokana na haki mwenye kugeuzwa.
-
10. Wazushi wameangamizwa.
-
11. Ambao wameghafilika katika ujinga.
-
12. Wanauliza: Ni lini hiyo siku ya malipo?
-
13. Hiyo ni siku watakayo adhibiwa Motoni.
-
14. Onjeni adhabu yenu! Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyahimiza.
-
15. Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.
-
16. Wanapokea aliyo wapa Mola wao Mlezi. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema.
-
17. Walikuwa wakilala kidogo tu usiku.
-
18. Na kabla ya alfajiri wakiomba maghfira.
-
19. Na katika mali yao ipo haki ya mwenye kuomba na asiye omba.
-
20. Na katika ardhi zipo Ishara kwa wenye yakini.
-
21. Na pia katika nafsi zenu - Je! Hamwoni?
-
22. Na katika mbingu ziko riziki zenu na mliyo ahidiwa.
-
23. Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, hakika haya ni kweli kama ilivyo kweli kuwa nyinyi mnasema.
-
24. Je! Imekufikia hadithi ya wageni wa Ibrahim wanao hishimiwa?
-
25. Walipo ingia kwake wakasema: Salama! Na yeye akasema: Salama! Nyinyi ni watu nisio kujueni.
-
26. Akenda kwa ahali yake na akaja na ndama aliye nona.
-
27. Akawakaribisha, akasema: Mbona hamli?
-
28. Akahisi kuwaogopa katika nafsi yake. Wakasema: Usiwe na khofu, nao wakambashiria kupata kijana mwenye ilimu.
-
29. Ndipo mkewe akawaelekea, na huku anasema na akijipiga usoni kwa mastaajabu, na kusema: Mimi ni kikongwe na tasa!
-
30. Wakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyo sema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mwenye kujua.
-
31. AKASEMA: Basi ujumbe wenu ni nini, enyi mlio tumwa?
-
32. Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa watu wakosefu,
-
33. Tuwatupie mawe ya udongo,
-
34. Yaliyo tiwa alama kutoka kwa Mola wako Mlezi kwa ajili ya wanao pindukia mipaka.
-
35. Kwa hivyo tutawatoa katika hao wale walio amini.
-
36. Lakini hatukupata humo ila nyumba moja tu yenye Waislamu!
-
37. Na tukaacha humo Ishara kwa ajili ya wanao iogopa adhabu chungu.
-
38. Na katika khabari za Musa, tulipo mtuma kwa Firauni na hoja wazi.
-
39. Lakini alipuuza kwa sababu ya nguvu zake na akasema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu!
-
40. Basi tukamkamata yeye na majeshi yake na tukawatupa baharini, na yeye ndiye wa kulaumiwa.
-
41. Na katika khabari za A`di tulipo wapelekea upepo wa kukata uzazi.
-
42. Haukuacha chochote ulicho kifikia ila ulikifanya kama kilio nyambuka.
-
43. Na katika khabari za Thamudi walipo ambiwa: Jifurahisheni kwa muda mdogo tu.
-
44. Wakaasi amri ya Mola wao Mlezi. Basi uliwanyakua moto wa radi nao wanaona.
-
45. Basi hawakuweza kusimama wala hawakuwa wenye kujitetea.
-
46. Na kaumu ya Nuhu hapo mbele. Hakika hao walikuwa watu wapotovu.
-
47. Na mbingu tumezifanya kwa nguvu na uwezo na hakika Sisi bila ya shaka ndio twenye uwezo wa kuzitanua.
-
48. Na ardhi tumeitandaza; basi watandazaji wazuri namna gani Sisi!
-
49. Na katika kila kitu tumeumba kwa jozi ili mzingatie.
-
50. Basi kimbilieni kwa Mwenyezi Mungu, hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.
-
51. Wala msifanye kuwa kuna mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.
-
52. Basi ndio hivyo hivyo, hakuwajia kabla yao Mtume ila walisema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu.
-
53. Je! Wameambizana kwa haya? Bali hawa ni watu waasi.
-
54. Basi waachilie mbali, nawe hulaumiwi.
-
55. Na kumbusha, kwani ukumbusho huwafaa Waumini.
-
56. Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi.
-
57. Na sitaki kwao riziki, wala sitaki wanilishe.
-
58. Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti.
-
59. Hakika walio dhulumu wana fungu lao la adhabu kama fungu la wenzao. Basi wasinihimize.
-
60. Ole wao walio ikanusha siku yao waliyo ahidiwa.
SHIRIKI
1
Al-Fatihah
2
Al Baqara
3
Ali `Imran
4
An-Nisa
5
Al-Ma`idah
6
Al-An`am
7
Al-A`raf
8
Al-Anfal
9
At-Tawbah
10
Yunus
11
Hud
12
Yusuf
13
Ar-Ra`d
14
Ibrahim
15
Al-Hijr
16
An-Nahl
17
Al-Isra
18
Al-Kahf
19
Maryam
20
Taha
21
Al-Anbya
22
Al-Haj
23
Al-Mu`minun
24
An-Nur
25
Al-Furqan
26
Ash-Shu`ara
27
An-Naml
28
Al-Qasas
29
Al-`Ankabut
30
Ar-Rum
31
Luqman
32
As-Sajdah
33
Al-Ahzab
34
Saba
35
Faatir
36
Ya-Sin
37
As-Saffat
38
Sad
39
Az-Zumar
40
Ghafir
41
Fussilat
42
sh-Shuraa
43
Az-Zukhruf
44
Ad-Dukhan
45
Al-Jathiyah
46
Al-Ahqaf
47
Muhammad
48
Al-Fath
49
Al-Hujurat
50
Qaf
51
Adh-Dhariyat
52
At-Tur
53
An-Najm
54
Al-Qamar
55
Ar-Rahman
56
Al-Waqi`ah
57
Al-Hadid
58
Al-Mujadila
59
Al-Hashr
60
Al-Mumtahanah
61
As-Saf
62
Al-Jumu`ah
63
Al-Munafiqun
64
At-Taghabun
65
At-Talaq
66
At-Tahrim
67
Al-Mulk
68
Al-Qalam
69
Al-Haqqah
70
Al-Ma`arij
71
Nuh
72
Al-Jinn
73
Al-Muzzammil
74
Al-Muddaththir
75
Al-Qiyamah
76
Al-Insan
77
Al-Mursalat
78
An-Naba
79
An-Nazi`at
80
Abasa
81
At-Takwir
82
Al-Infitar
83
Al-Mutaffifin
84
Al-Inshiqaq
85
Al-Buruj
86
At-Tariq
87
Al-A`la
88
Al-Ghashiyah
89
Al-Fajr
90
Al-Balad
91
Ash-Shams
92
Al-Layl
93
Ad-Duhaa
94
Ash-Sharh
95
At-Tin
96
Al-`Alaq
97
Al-Qadr
98
Al-Bayyinah
99
Az-Zalzalah
100
Al-`Adiyat
101
Al-Qari`ah
102
At-Takathur
103
Al-`Asr
104
Al-Humazah
105
Al-Fil
106
Quraysh
107
Al-Ma`un
108
Al-Kawthar
109
Al-Kafirun
110
An-Nasr
111
Al-Masad
112
Al-Ikhlas
113
Al-Falaq
114
An-Nas