87. Al-A`la - Qurani
- 1. Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa,
- 2. Aliye umba, na akaweka sawa,
- 3. Na ambaye amekadiria na akaongoa,
- 4. Na aliye otesha malisho,
- 5. Kisha akayafanya makavu, meusi.
- 6. Tutakusomesha wala hutasahau,
- 7. Ila akipenda Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahiri na yaliyo fichikana.
- 8. Na tutakusahilishia yawe mepesi.
- 9. Basi kumbusha, kama kukumbusha kunafaa.
- 10. Atakumbuka mwenye kuogopa.
- 11. Na atajitenga mbali nayo mpotovu,
- 12. Ambaye atauingia Moto mkubwa.
- 13. Tena humo hatakufa wala hawi hai.
- 14. Hakika amekwisha fanikiwa aliye jitakasa.
- 15. Na akakumbuka jina la Mola wake Mlezi, na akasali.
- 16. Lakini nyinyi mnakhiari maisha ya dunia!
- 17. Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi.
- 18. Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo,
- 19. Vitabu vya Ibrahimu na Musa.