87. Al-A`la - Qurani
- 1. Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa,
- 2. Aliye umba, na akaweka sawa,
- 3. Na ambaye amekadiria na akaongoa,
- 4. Na aliye otesha malisho,
- 5. Kisha akayafanya makavu, meusi.
- 6. Tutakusomesha wala hutasahau,
- 7. Ila akipenda Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahiri na yaliyo fichikana.
- 8. Na tutakusahilishia yawe mepesi.
- 9. Basi kumbusha, kama kukumbusha kunafaa.