• 1. Naapa kwa tini na zaituni!

  • 2. Na kwa Mlima wa Sinai!

  • 3. Na kwa mji huu wenye amani!

  • 4. Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa.

  • 5. Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini!

  • 6. Lakini wale walio amini na wakatenda mema, hao watapata ujira usio kwisha.

  • 7. Basi ni kipi baadaye kitacho kukukadhibishia malipo?

  • 8. Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu kuliko mahakimu wote?