• 1. Hakika Sisi tumeiteremsha Qur`ani katika Laylatul Qadri, Usiku wa Cheo Kitukufu.

  • 2. Na nini kitacho kujuulisha nini Laylatul Qadri?

  • 3. Laylatul Qadri ni bora kuliko miezi elfu.

  • 4. Huteremka Malaika na Roho katika usiku huo kwa idhini ya Mola wao Mlezi kwa kila jambo.

  • 5. Amani usiku huo mpaka mapambazuko ya alfajiri.