15. Al-Hijr - Qurani
- 1. Alif Lam Ra. (A. L. R). Hizi ni Aya za Kitabu na Qur`ani inayo bainisha.
- 2. HUENDA ikawa walio kufuru wakatamani wange kuwa Waislamu.
- 3. Waache wale, na wastarehe, na iwazuge tamaa. Watakuja jua.
- 4. Na hatukuuangamiza mji wowote ule ila ulikuwa na muda wake maalumu.
- 5. Hawawezi watu wowote kuitangulia ajali yao, wala kuchelewa.
- 6. Na walisema: Ewe uliyeteremshiwa Ukumbusho! Hakika wewe ni mwendawazimu.
- 7. Mbona hutuletei Malaika ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli?
- 8. Sisi hatuwateremshi Malaika ila kwa sababu ya haki, na hapo hawatapewa muhula.
- 9. Hakika Sisi ndio tulio teremsha Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio tutao ulinda.