Al-Hijr - QURAN - Harun Yahya
-
1. Alif Lam Ra. (A. L. R). Hizi ni Aya za Kitabu na Qur`ani inayo bainisha.
-
2. HUENDA ikawa walio kufuru wakatamani wange kuwa Waislamu.
-
3. Waache wale, na wastarehe, na iwazuge tamaa. Watakuja jua.
-
4. Na hatukuuangamiza mji wowote ule ila ulikuwa na muda wake maalumu.
-
5. Hawawezi watu wowote kuitangulia ajali yao, wala kuchelewa.
-
6. Na walisema: Ewe uliyeteremshiwa Ukumbusho! Hakika wewe ni mwendawazimu.
-
7. Mbona hutuletei Malaika ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli?
-
8. Sisi hatuwateremshi Malaika ila kwa sababu ya haki, na hapo hawatapewa muhula.
-
9. Hakika Sisi ndio tulio teremsha Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio tutao ulinda.
-
10. Na hakika tulikwisha watumia Mitume mataifa ya mwanzo.
-
11. Na hakuwafikia Mtume ila walimkejeli.
-
12. Na kama hivi ndivyo tunavyo ingiza katika nyoyo za wakosefu.
-
13. Hawayaamini haya, na hali ya kuwa umekwisha wapitia mfano wa watu wa kale.
-
14. Na lau tungeli wafungulia mlango wa mbingu, wakawa wanapanda,
-
15. Basi wangeli sema: Macho yetu yamelevywa, bali sisi wenyewe tumerogwa.
-
16. Na hakika tumeweka katika mbingu vituo vya sayari, na tumezipamba kwa wenye kuangalia.
-
17. Na tumezilinda na kila shetani afukuzwaye.
-
18. Isipo kuwa mwenye kusikiliza kwa kuibia, naye hufuatwa na kijinga cha moto kinacho onekana.
-
19. Na ardhi tumeitandaza na humo tumeweka milima, na tumeotesha kila kitu kwa kiasi chake.
-
20. Na tumekujaalieni humo vitu vya maisha yenu, na ya hao ambao nyinyi sio wenye kuwaruzuku.
-
21. Na hakuna chochote ila asili yake inatokana na Sisi; wala hatukiteremshi ila kwa kipimo maalumu.
-
22. Na tunazipeleka pepo za kupandishia, na tunateremsha kutoka mbinguni maji, kisha tukakunywesheni maji hayo. Wala si nyinyi mnayo yaweka.
-
23. Na Sisi ndio tunao huisha na tunao fisha. Na Sisi ndio Warithi.
-
24. Na tunawajua walio tangulia katika nyinyi, na tunawajua walio taakhari.
-
25. Na hakika Mola wako Mlezi ndiye atakaye wakusanya. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mjuzi.
-
26. Na tulimuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.
-
27. Na majini tuliwaumba kabla kwa moto wa upepo umoto.
-
28. Na Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.
-
29. Basi nitakapo mkamilisha na nikampulizia roho yangu, basi mumwangukie kumsujudia.
-
30. Basi Malaika wote pamoja walimsujudia,
-
31. Isipo kuwa Iblisi. Yeye alikataa kuwa pamoja na walio sujudu.
-
32. (Mwenyezi Mungu) akasema: Ewe Iblisi! Una nini hata hukuwa pamoja na walio sujudu?
-
33. Akasema: Haiwi mimi nimsujudie mtu uliye muumba kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yenye sura.
-
34. (Mwenyezi Mungu) akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe ni maluuni!
-
35. Na hakika juu yako ipo laana mpaka Siku ya Malipo.
-
36. Akasema (Iblisi): Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watapo fufuliwa.
-
37. (Mwenyezi Mungu) akasema: Hakika wewe ni katika walio pewa muhula
-
38. Mpaka siku ya wakati maalumu.
-
39. Akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyo kuwa umenitia makosani, basi nahakikisha nitawazaini hapa duniani na nitawapoteza wote,
-
40. Ila waja wako walio safika.
-
41. Akasema: Hii Njia ya kujia kwangu Iliyo Nyooka.
-
42. Hakika waja wangu, wewe hutakuwa na mamlaka juu yao, isipo kuwa wale wapotofu walio kufuata.
-
43. Na bila shaka Jahannamu ndipo pahali pao walipo ahidiwa wote.
-
44. Ina milango saba; na kwa kila mlango iko sehemu walio tengewa.
-
45. Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.
-
46. (Wataambiwa:) Ingieni kwa salama na amani.
-
47. Na tutaondoa chuki iliyo kuwamo vifuani mwao, wawe ndugu juu ya viti vya enzi wameelekeana.
-
48. Humo hayatawagusa machofu, wala hawatatolewa humo.
-
49. Waambie waja wangu ya kwamba Mimi ndiye Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.
-
50. Na kwamba adhabu yangu ndio adhabu iliyo chungu!
-
51. Na uwape khabari za wageni wa Ibrahim.
-
52. Walipo ingia kwake na wakasema: Salama! Yeye akasema: Hakika sisi tunakuogopeni.
-
53. Wakasema: Usiogope. Sisi tunakubashiria kijana mwenye ujuzi.
-
54. Akasema: Mnanibashiria nami uzee umenishika! Basi kwa njia gani mnanibashiria?
-
55. Wakasema: Tunakubashiria kwa haki; basi usiwe miongoni mwa wanao kata tamaa.
-
56. Akasema: Na nani anaye kata tamaa na rehema ya Mola wake Mlezi ila wale walio potea?
-
57. Akasema: Hebu nini amri yenu, enyi wajumbe?
-
58. Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa kaumu ya wakosefu!
-
59. Isipo kuwa walio mfuata Luut`i. Bila ya shaka sisi tutawaokoa hao wote.
-
60. Ila mkewe. Tunakadiria huyo atakuwa miongoni watao bakia nyuma.
-
61. Basi wale wajumbe walipo fika kwa Luut`i,
-
62. Alisema (Luut`i): Hakika nyinyi ni watu msio juulikana.
-
63. Wakasema: Bali sisi tumekuletea yale waliyo kuwa wakiyafanyia shaka.
-
64. Na tumefika kwako kwa Haki, na hakika sisi tunasema kweli.
-
65. Basi ondoka na ahli zako usiku ungalipo, nawe ufuate nyuma yao, wala yeyote kati yenu asigeuke nyuma. Na mwende mnapo amrishwa.
-
66. Na tukamfunulia hukumu hiyo, ya kwamba hata wa mwisho wao hao ikifika asubuhi atakuwa kesha katiliwa mbali.
-
67. Na wakaja watu wa mji ule nao furahani.
-
68. Akasema: Hakika hawa wageni wangu, basi msinifedheheshe.
-
69. Na mcheni Mwenyezi Mungu, wala msinihizi.
-
70. Wakasema: Sisi hatukukukataza usimkaribishe yeyote?
-
71. Akasema: Hawa binti zangu, ikiwa nyinyi ni watendaji.
-
72. Naapa kwa umri wako! Hakika hao walikuwa katika ulevi wao, wakihangaika ovyo.
-
73. Ukelele ukawatwaa wakipambaukiwa.
-
74. Na tukaigeuza nchi juu chini, na tukawanyeshea mvua ya mawe ya udongo wa Motoni.
-
75. Hakika katika hayo zipo ishara kwa waaguzi.
-
76. Na miji hii ipo kwenye njia inayo pitiwa.
-
77. Hakika katika hayo ipo ishara kwa Waumini.
-
78. Na hakika watu wa Kichakani walikuwa wenye kudhulumu.
-
79. Kwa hivyo tukawaadhibu. Na nchi mbili hizi ziko kwenye njia ilio wazi.
-
80. Na bila ya shaka wakaazi wa Hijr waliwakanusha Mitume.
-
81. Na tuliwapa ishara zetu, nao wakazipuuza.
-
82. Nao walikuwa wakichonga majumba katika milima kwa amani.
-
83. Basi ukelele ukawatwaa asubuhi.
-
84. Hayakuwafaa waliyo kuwa wakiyachuma.
-
85. Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake ila kwa ajili ya Haki. Na hakika Kiyama kitafika. Basi samehe msamaha mzuri.
-
86. Hakika Mola wako Mlezi ndiye Muumbaji Mjuzi.
-
87. Na tumekupa Aya saba zinazo somwa mara kwa mara, na Qur`ani Tukufu.
-
88. Usivitumbulie macho yako vitu tulivyo waneemesha makundi fulani kati yao, wala usiwahuzunikie. Na wainamishie bawa lako (la huruma) Waumini.
-
89. Na sema: Hakika mimi ni mwonyaji mwenye kubainisha.
-
90. Kama hivyo tuliwateremshia walio gawa,
-
91. Ambao wakaifanya Qur`ani vipande vipande.
-
92. Basi Naapa kwa Mola wako Mlezi! Tutawahoji wote,
-
93. Kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
-
94. Basi wewe yatangaze uliyo amrishwa, na jitenge na washirikina.
-
95. Hakika Sisi tunatosha kukukinga na wanao kejeli.
-
96. Hao wanao fanya kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu yupo mungu mwingine. Basi, watakuja jua!
-
97. Na Sisi tunajua kwa hakika kuwa wewe kifua chako kinaona dhiki kwa hayo wayasemayo.
-
98. Basi mtakase Mola wako Mlezi kwa kumhimidi, na uwe miongoni wanao msujudia.
-
99. Na muabudu Mola wako Mlezi mpaka ikufikie Yakini.
SHIRIKI
1
Al-Fatihah
2
Al Baqara
3
Ali `Imran
4
An-Nisa
5
Al-Ma`idah
6
Al-An`am
7
Al-A`raf
8
Al-Anfal
9
At-Tawbah
10
Yunus
11
Hud
12
Yusuf
13
Ar-Ra`d
14
Ibrahim
15
Al-Hijr
16
An-Nahl
17
Al-Isra
18
Al-Kahf
19
Maryam
20
Taha
21
Al-Anbya
22
Al-Haj
23
Al-Mu`minun
24
An-Nur
25
Al-Furqan
26
Ash-Shu`ara
27
An-Naml
28
Al-Qasas
29
Al-`Ankabut
30
Ar-Rum
31
Luqman
32
As-Sajdah
33
Al-Ahzab
34
Saba
35
Faatir
36
Ya-Sin
37
As-Saffat
38
Sad
39
Az-Zumar
40
Ghafir
41
Fussilat
42
sh-Shuraa
43
Az-Zukhruf
44
Ad-Dukhan
45
Al-Jathiyah
46
Al-Ahqaf
47
Muhammad
48
Al-Fath
49
Al-Hujurat
50
Qaf
51
Adh-Dhariyat
52
At-Tur
53
An-Najm
54
Al-Qamar
55
Ar-Rahman
56
Al-Waqi`ah
57
Al-Hadid
58
Al-Mujadila
59
Al-Hashr
60
Al-Mumtahanah
61
As-Saf
62
Al-Jumu`ah
63
Al-Munafiqun
64
At-Taghabun
65
At-Talaq
66
At-Tahrim
67
Al-Mulk
68
Al-Qalam
69
Al-Haqqah
70
Al-Ma`arij
71
Nuh
72
Al-Jinn
73
Al-Muzzammil
74
Al-Muddaththir
75
Al-Qiyamah
76
Al-Insan
77
Al-Mursalat
78
An-Naba
79
An-Nazi`at
80
Abasa
81
At-Takwir
82
Al-Infitar
83
Al-Mutaffifin
84
Al-Inshiqaq
85
Al-Buruj
86
At-Tariq
87
Al-A`la
88
Al-Ghashiyah
89
Al-Fajr
90
Al-Balad
91
Ash-Shams
92
Al-Layl
93
Ad-Duhaa
94
Ash-Sharh
95
At-Tin
96
Al-`Alaq
97
Al-Qadr
98
Al-Bayyinah
99
Az-Zalzalah
100
Al-`Adiyat
101
Al-Qari`ah
102
At-Takathur
103
Al-`Asr
104
Al-Humazah
105
Al-Fil
106
Quraysh
107
Al-Ma`un
108
Al-Kawthar
109
Al-Kafirun
110
An-Nasr
111
Al-Masad
112
Al-Ikhlas
113
Al-Falaq
114
An-Nas