• 1. Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba,

  • 2. Amemuumba binaadamu kwa tone la damu,

  • 3. Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote!

  • 4. Ambaye amefundisha kwa kalamu.

  • 5. Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui.

  • 6. Kwani! Hakika mtu bila ya shaka huwa jeuri

  • 7. Akijiona katajirika.

  • 8. Hakika kwa Mola wako Mlezi ndio marejeo.

  • 9. Umemwona yule anaye mkataza

  • 10. Mja anapo sali?

  • 11. Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu?

  • 12. Au anaamrisha uchamngu?

  • 13. Umeona kama yeye akikanusha na anarudi nyuma?

  • 14. Hajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anaona?

  • 15. Kwani! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la nywele!

  • 16. Shungi la uwongo, lenye makosa!

  • 17. Basi na awaite wenzake!

  • 18. Nasi tutawaita Mazabania!

  • 19. Hasha! Usimt`ii! Nawe sujudu na ujongee!