84. Al-Inshiqaq - Qurani
- 1. Itapo chanika mbingu,
- 2. Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
- 3. Na ardhi itakapo tanuliwa,
- 4. Na kuvitoa vilivyo kuwa ndani yake, ikawa tupu,
- 5. Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
- 6. Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta.
- 7. Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia,
- 8. Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi,
- 9. Na arudi kwa ahali zake na furaha.