• 1. Itapo chanika mbingu,

  • 2. Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,

  • 3. Na ardhi itakapo tanuliwa,

  • 4. Na kuvitoa vilivyo kuwa ndani yake, ikawa tupu,

  • 5. Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,

  • 6. Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta.

  • 7. Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia,

  • 8. Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi,

  • 9. Na arudi kwa ahali zake na furaha.

  • 10. Na ama atakaye pewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake,

  • 11. Basi huyo ataomba kuteketea.

  • 12. Na ataingia Motoni.

  • 13. Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake.

  • 14. Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena.

  • 15. Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona!

  • 16. Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapo kuchwa,

  • 17. Na kwa usiku na unavyo vikusanya,

  • 18. Na kwa mwezi unapo pevuka,

  • 19. Lazima mtapanda t`abaka kwa t`abaka!

  • 20. Basi wana nini hawaamini?

  • 21. Na wanapo somewa Qur`ani hawasujudu?

  • 22. Bali walio kufuru wanakanusha tu.

  • 23. Na Mwenyezi Mungu anajua wanayo yadhamiria.

  • 24. Basi wabashirie adhabu chungu!

  • 25. Isipo kuwa wale walio amini na wakatenda mema; hao watakuwa na ujira usio malizika.