Ash-Shu`ara - QURAN - Harun Yahya
-
1. T`aa Siin Miim. (T`. S. M.)
-
2. Hizi ni Aya za Kitabu kinacho bainisha.
-
3. Huenda labda ukajikera nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini.
-
4. Tunge penda tungeli wateremshia kutoka mbinguni Ishara zikanyenyekea shingo zao.
-
5. Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman ila wao hujitenga nao.
-
6. Kwa yakini wamekanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia khabari za yale waliyo kuwa wakiyafanyia mzaha.
-
7. Je! Hawakuiona ardhi, mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri?
-
8. Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
-
9. Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
-
10. Na Mola wako Mlezi, alipo mwita Musa, akamwambia: Fika kwa watu madhaalimu,
-
11. Watu wa Firauni. Hawaogopi?
-
12. Akasema: Hakika mimi nachelea wasinikanushe.
-
13. Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun.
-
14. Na wao wana kisasi juu yangu, kwa hivyo naogopa wasije kuniuwa.
-
15. Akasema: Siyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza.
-
16. Basi mfikieni Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
-
17. Waachilie Wana wa Israili wende nasi.
-
18. (Firauni) akasema: Sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa kwetu katika umri wako miaka mingi?
-
19. Na ukatenda kitendo chako ulicho tenda, nawe ukawa miongoni mwa wasio na shukrani?
-
20. (Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipo kuwa miongoni mwa wale walio potea.
-
21. Basi nikakukimbieni nilipo kuogopeni, tena Mola wangu Mlezi akanitunukia hukumu, na akanijaalia niwe miongoni mwa Mitume.
-
22. Na hiyo ndiyo neema ya kunisumbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili?
-
23. Firauni akasema: Na nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote?
-
24. Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi ni wenye yakini.
-
25. (Firauni) akawaambia walio mzunguka: Hamsikilizi?
-
26. (Musa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza.
-
27. (Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliye tumwa kwenu ni mwendawazimu.
-
28. (Musa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi mnatia akilini.
-
29. (Firauni) akasema: Ukimfuata mungu mwengine asiye kuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani.
-
30. Akasema: Je! Ijapo kuwa nitakuletea kitu cha kubainisha wazi?
-
31. Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wasemao kweli.
-
32. Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhaahiri.
-
33. Na akautoa mkono wake, na mara ukawa mweupe kwa watazamao.
-
34. (Firauni) akawaambia waheshimiwa walio mzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu.
-
35. Anataka kukutoeni katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?
-
36. Wakasema: Mpe muda yeye na nduguye na uwatume mijini wapigao mbiu ya mgambo.
-
37. Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu.
-
38. Basi wakakusanywa wachawi wakati na siku maalumu.
-
39. Na watu wakaambiwa: Je! Mtakusanyika?
-
40. Huenda tutawafuata wachawi wakiwa wao ndio watakao shinda.
-
41. Basi walipo kuja wachawi wakamwambia Firauni: Je! Tutapata ujira tukiwa sisi ndio tulio shinda?
-
42. Naam! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele.
-
43. Musa akwaambia: Tupeni mnavyo taka kutupa.
-
44. Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda.
-
45. Musa tena akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza walivyo vizua.
-
46. Hapo wachawi walipinduka wakasujudu.
-
47. Wakasema: Tunamuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote.
-
48. Mola Mlezi wa Musa na Harun.
-
49. (Firauni) akasema: Je! Mmemuamini kabla sijakuruhusuni? Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliye kufunzeni uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutafautisha. Na nitakubandikeni misalabani nyote.
-
50. Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
-
51. Hakika sisi tunatumai Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa ndio wa kwanza wa kuamini.
-
52. Na tulimuamrisha Musa kwa wahyi: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika mtafuatwa.
-
53. Basi Firauni akawatuma mijini wapiga mbiu za mgambo.
-
54. (Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo.
-
55. Nao wanatuudhi.
-
56. Na sisi ni wengi, wenye kuchukua hadhari.
-
57. Basi tukawatoa katika mabustani na chemchem,
-
58. Na makhazina, na vyeo vya hishima,
-
59. Kadhaalika; na tukawarithisha hayo Wana wa Israili.
-
60. Basi wakawafuata lilipo chomoza jua.
-
61. Na yalipo onana majeshi mawili haya, watu wa Musa wakasema: Hakika sisi bila ya shaka tumepatikana!
-
62. (Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa!
-
63. Tulimletea wahyi Musa tukamwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa.
-
64. Na tukawajongeza hapo wale wengine.
-
65. Tukawaokoa Musa na walio kuwa pamoja naye wote.
-
66. Kisha tukawazamisha hao wengine.
-
67. Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara; lakini wengi wao si katika wenye kuamini.
-
68. Na kwa hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
-
69. Na wasomee khabari za Ibrahim.
-
70. Alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?
-
71. Wakasema: Tunaabudu masanamu, daima tunayanyenyekea.
-
72. Akasema: Je! Yanakusikieni mnapo yaita?
-
73. Au yanakufaeni, au yanakudhuruni?
-
74. Wakasema: Bali tumewakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo.
-
75. Je! Mmewaona hawa mnao waabudu-
-
76. Nyinyi na baba zenu wa zamani?
-
77. Kwani hakika hao ni adui zangu, isipo kuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
-
78. Ambaye ndiye aliye niumba, na Yeye ndiye ananiongoa,
-
79. Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha.
-
80. Na ninapo ugua ni Yeye ndiye anaye niponesha.
-
81. Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha.
-
82. Na ambaye ndiye ninaye mtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo.
-
83. Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na watendao mema.
-
84. Na unijaalie nitajwe kwa wema na watu watakao kuja baadaye.
-
85. Na unijaalie katika warithi wa Bustani za neema.
-
86. Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu.
-
87. Wala usinihizi Siku watapo fufuliwa.
-
88. Siku ambayo kwamba mali hayato faa kitu wala wana.
-
89. Isipo kuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi.
-
90. Na Pepo itasogezwa kwa wachamngu.
-
91. Na Jahannamu itadhihirishwa kwa wapotovu.
-
92. Na wataambiwa: Wako wapi mlio kuwa mkiwaabudu
-
93. Badala ya Mwenyezi Mungu? Je! Wanakusaidieni, au wanajisaidia wenyewe?
-
94. Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu,
-
95. Na majeshi ya Ibilisi yote.
-
96. Watasema, na hali ya kuwa wanazozana humo:
-
97. Wallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu ulio dhaahiri,
-
98. Tulipo kufanyeni ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote.
-
99. Na hawakutupoteza ila wale wakosefu.
-
100. Basi hatuna waombezi.
-
101. Wala rafiki wa dhati.
-
102. Laiti tungeli pata kurejea tena tungeli kuwa katika Waumini.
-
103. Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
-
104. Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
-
105. Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume.
-
106. Alipo waambia ndugu yao, Nuhu: Je! Hamchimngu?
-
107. Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
-
108. Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit`iini mimi.
-
109. Na sikutakini juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
-
110. Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit`iini mimi.
-
111. Wakasema: Je! Tukuamini wewe, hali wanao kufuata ni watu wa chini?
-
112. Akasema: Nayajuaje waliyo kuwa wakiyafanya?
-
113. Hisabu yao haiko ila kwa Mola wao Mlezi, laiti mngeli tambua!
-
114. Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini.
-
115. Mimi si cho chote ila ni Mwonyaji wa dhaahiri shaahiri.
-
116. Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe.
-
117. Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikanusha.
-
118. Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami, Waumini.
-
119. Kwa hivyo tukamwokoa yeye na walio kuwa pamoja naye katika marikebu iliyo sheheni.
-
120. Kisha tukawazamisha baadaye walio bakia.
-
121. Hakika katika haya ipo Ishara, lakini si wengi wao walio kuwa Waumini.
-
122. Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
-
123. Kina A`d waliwakanusha Mitume.
-
124. Alipo waambia ndugu yao, Hud: Je! Hamchimngu?
-
125. Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
-
126. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit`iini mimi.
-
127. Wala sikutakeni juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
-
128. Je! Mnajenga juu ya kila mnyanyuko kumbusho la kufanyia upuuzi?
-
129. Na mnajenga majengo ya fakhari kama kwamba mtaishi milele!
-
130. Na mnapo tumia nguvu mnatumia nguvu kwa ujabari.
-
131. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit`iini.
-
132. Na mcheni aliye kupeni haya mnayo yajua.
-
133. Amekupeni wanyama wa kufuga na wana.
-
134. Na mabustani na chemchem.
-
135. Hakika mimi ninakukhofieni adhabu ya Siku Kubwa.
-
136. Wakasema: Ni mamoja kwetu, ukitupa mawaidha au hukuwa miongoni mwa watoao mawaidha.
-
137. Haya si chochote ila ni mtindo wa watu wa tokea zamani.
-
138. Wala sisi hatutaadhibiwa.
-
139. Wakamkanusha; nasi tukawaangamiza. Hakika bila ya shaka katika haya ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
-
140. Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
-
141. Kina Thamud waliwakanusha Mitume.
-
142. Alipo waambia ndugu yao Saleh: Je! Hamumchimngu?
-
143. Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
-
144. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit`iini.
-
145. Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
-
146. Je! Mtaachwa salama usalimina katika haya yaliyopo hapa?
-
147. Katika mabustani, na chemchem?
-
148. Na konde na mitende yenye makole yaliyo wiva.
-
149. Na mnachonga milimani majumba kwa ustadi.
-
150. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit`iini mimi.
-
151. Wala msit`ii amri za walio pindukia mipaka,
-
152. Ambao wanafanya ufisadi katika nchi, wala hawatengenezi.
-
153. Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa walio rogwa.
-
154. Wewe si chochote ila ni mtu kama sisi. Basi lete Ishara ukiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.
-
155. Akasema: Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa, na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalumu.
-
156. Wala msimguse kwa uwovu, isije ikakushikeni adhabu ya Siku Kubwa.
-
157. Lakini wakamuuwa, na wakawa wenye kujuta.
-
158. Basi ikawapata adhabu. Hakika katika hayo ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
-
159. Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
-
160. Watu wa Lut`i waliwakanusha Mitume.
-
161. Alipo waambia ndugu yao, Lut`i: Je! Hamumchimngu?
-
162. Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu kwenu.
-
163. Basi mcheni Mwenyezi Mungu na nit`iini mimi.
-
164. Wala mimi sikutakini ujira juu yake; ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
-
165. Je! Katika viumbe vyote mnawaingilia wanaume?
-
166. Na mnaacha alicho kuumbieni Mola wenu Mlezi katika wake zenu? Ama kweli nyinyi ni watu mnao ruka mipaka!
-
167. Wakasema: Ewe Lut`i! Usipo acha, hapana shaka utakuwa miongoni mwa wanao tolewa mji!
-
168. Akasema: Hakika mimi ni katika wanao kichukia hichi kitendo chenu.
-
169. Mola wangu Mlezi! Niokoe mimi na ahali zangu na haya wayatendayo.
-
170. Basi tukamwokoa yeye na ahali zake wote,
-
171. Isipo kuwa kikongwe katika walio kaa nyuma.
-
172. Kisha tukawaangamiza wale wengine.
-
173. Na tukawanyeshea mvua, basi ni ovu mno mvua ya waliyo onywa.
-
174. Hakika katika hayo ipo Ishara. Na hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
-
175. Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
-
176. Watu wa Machakani waliwakanusha Mitume.
-
177. Shuaibu alipo waambia: Je! Hamfanyi mkamchamngu?
-
178. Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
-
179. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit`iini mimi.
-
180. Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
-
181. Timizeni kipimo sawa sawa, wala msiwe katika wanao punja.
-
182. Na pimeni kwa haki iliyo nyooka;
-
183. Wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye jeuri kwa ufisadi.
-
184. Na mcheni aliye kuumbeni nyinyi na vizazi vilivyo tangulia.
-
185. Wakasema: Hakika wewe ni katika walio rogwa.
-
186. Na wewe si chochote ila ni mtu tu kama sisi, na kwa yakini tunakuona wewe ni katika waongo.
-
187. Hebu tuangushie vipande kutoka mbinguni ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.
-
188. Akasema: Mola wangu Mlezi anajua zaidi mnayo yatenda.
-
189. Basi walimkanusha, na ikawashika adhabu ya siku ya kivuli. Hakika hiyo ilikuwa adhabu ya siku kubwa.
-
190. Hakika katika hayo ipo Ishara, lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
-
191. Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
-
192. Na bila ya shaka hii ni Uteremsho wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
-
193. Ameuteremsha Roho muaminifu,
-
194. Juu ya moyo wako, ili uwe katika Waonyaji,
-
195. Kwa ulimi wa Kiarabu ulio wazi.
-
196. Na hakika bila ya shaka haya yamo katika Vitabu vya kale.
-
197. Je! Haikuwa kwao ni Ishara kwamba wanayajua haya wanazuoni wa Wana wa Israili?
-
198. Na lau kuwa tungeli iteremsha juu ya mmoja wa wasio kuwa Waarabu,
-
199. Na akawasomea, wasingeli kuwa wenye kuamini.
-
200. Namna hivi tunaingiza katika nyoyo za wakosefu.
-
201. Hawataiamini mpaka waione adhabu chungu.
-
202. Basi itawafikia kwa ghafla, na hali hawana khabari.
-
203. Na watasema: Je, tutapewa muhula?
-
204. Basi, je, wanaihimiza adhabu yetu?
-
205. Waonaje kama tukiwastarehesha kwa miaka,
-
206. Kisha yakawafikia waliyo kuwa wakiahidiwa,
-
207. Yatawafaa nini yale waliyo stareheshewa?
-
208. Wala hatukuangamiza mji wo wote ila ulikuwa na waonyaji -
-
209. Kuwa ni ukumbusho. Wala Sisi hatukuwa wenye kudhulumu.
-
210. Wala Mashet`ani hawakuteremka nayo,
-
211. Wala haitakiwi kwao, na wala hawawezi.
-
212. Hakika hao wametengwa na kusikia.
-
213. Basi usimwombe mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu ukawa miongoni mwa watakao adhibiwa.
-
214. Na uwaonye jamaa zako walio karibu nawe.
-
215. Na watwae kwa upole wanao kufuata miongoni mwa Waumini.
-
216. Na ikiwa watakuasi basi sema: Mimi najitenga mbali na hayo mnayo yatenda.
-
217. Na umtegemee Mtukufu Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
-
218. Ambaye anakuona unapo simama,
-
219. Na mageuko yako kati ya wanao sujudu.
-
220. Hakika Yeye ndiye Mwenye kusikia Mwenye kujua.
-
221. Je! Nikwambieni nani wanawashukia Mashet`ani?
-
222. Wanamshukia kila mzushi mkubwa mwingi wa dhambi.
-
223. Wanawapelekea yale wanayo yasikia; na wengi wao ni waongo.
-
224. Na watungaji mashairi ni wapotofu ndio wanawafuata.
-
225. Je! Huwaoni kwamba wao wanatangatanga katika kila bonde?
-
226. Na kwamba wao husema wasiyo yatenda?
-
227. Isipo kuwa wale walio amini, na wakatenda mema, na wakamkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi, na wakajitetea wanapo dhulumiwa. Na wanao dhulumu watakuja jua mgeuko gani watakao geuka.
SHIRIKI
1
Al-Fatihah
2
Al Baqara
3
Ali `Imran
4
An-Nisa
5
Al-Ma`idah
6
Al-An`am
7
Al-A`raf
8
Al-Anfal
9
At-Tawbah
10
Yunus
11
Hud
12
Yusuf
13
Ar-Ra`d
14
Ibrahim
15
Al-Hijr
16
An-Nahl
17
Al-Isra
18
Al-Kahf
19
Maryam
20
Taha
21
Al-Anbya
22
Al-Haj
23
Al-Mu`minun
24
An-Nur
25
Al-Furqan
26
Ash-Shu`ara
27
An-Naml
28
Al-Qasas
29
Al-`Ankabut
30
Ar-Rum
31
Luqman
32
As-Sajdah
33
Al-Ahzab
34
Saba
35
Faatir
36
Ya-Sin
37
As-Saffat
38
Sad
39
Az-Zumar
40
Ghafir
41
Fussilat
42
sh-Shuraa
43
Az-Zukhruf
44
Ad-Dukhan
45
Al-Jathiyah
46
Al-Ahqaf
47
Muhammad
48
Al-Fath
49
Al-Hujurat
50
Qaf
51
Adh-Dhariyat
52
At-Tur
53
An-Najm
54
Al-Qamar
55
Ar-Rahman
56
Al-Waqi`ah
57
Al-Hadid
58
Al-Mujadila
59
Al-Hashr
60
Al-Mumtahanah
61
As-Saf
62
Al-Jumu`ah
63
Al-Munafiqun
64
At-Taghabun
65
At-Talaq
66
At-Tahrim
67
Al-Mulk
68
Al-Qalam
69
Al-Haqqah
70
Al-Ma`arij
71
Nuh
72
Al-Jinn
73
Al-Muzzammil
74
Al-Muddaththir
75
Al-Qiyamah
76
Al-Insan
77
Al-Mursalat
78
An-Naba
79
An-Nazi`at
80
Abasa
81
At-Takwir
82
Al-Infitar
83
Al-Mutaffifin
84
Al-Inshiqaq
85
Al-Buruj
86
At-Tariq
87
Al-A`la
88
Al-Ghashiyah
89
Al-Fajr
90
Al-Balad
91
Ash-Shams
92
Al-Layl
93
Ad-Duhaa
94
Ash-Sharh
95
At-Tin
96
Al-`Alaq
97
Al-Qadr
98
Al-Bayyinah
99
Az-Zalzalah
100
Al-`Adiyat
101
Al-Qari`ah
102
At-Takathur
103
Al-`Asr
104
Al-Humazah
105
Al-Fil
106
Quraysh
107
Al-Ma`un
108
Al-Kawthar
109
Al-Kafirun
110
An-Nasr
111
Al-Masad
112
Al-Ikhlas
113
Al-Falaq
114
An-Nas