35. Anataka kukutoeni katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?
36. Wakasema: Mpe muda yeye na nduguye na uwatume mijini wapigao mbiu ya mgambo.
37. Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu.
38. Basi wakakusanywa wachawi wakati na siku maalumu.
39. Na watu wakaambiwa: Je! Mtakusanyika?
40. Huenda tutawafuata wachawi wakiwa wao ndio watakao shinda.
41. Basi walipo kuja wachawi wakamwambia Firauni: Je! Tutapata ujira tukiwa sisi ndio tulio shinda?
42. Naam! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele.
43. Musa akwaambia: Tupeni mnavyo taka kutupa.
44. Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda.
45. Musa tena akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza walivyo vizua.
46. Hapo wachawi walipinduka wakasujudu.
47. Wakasema: Tunamuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote.
48. Mola Mlezi wa Musa na Harun.
49. (Firauni) akasema: Je! Mmemuamini kabla sijakuruhusuni? Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliye kufunzeni uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutafautisha. Na nitakubandikeni misalabani nyote.
50. Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
51. Hakika sisi tunatumai Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa ndio wa kwanza wa kuamini.
52. Na tulimuamrisha Musa kwa wahyi: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika mtafuatwa.
53. Basi Firauni akawatuma mijini wapiga mbiu za mgambo.
54. (Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo.
55. Nao wanatuudhi.
56. Na sisi ni wengi, wenye kuchukua hadhari.
57. Basi tukawatoa katika mabustani na chemchem,
58. Na makhazina, na vyeo vya hishima,
59. Kadhaalika; na tukawarithisha hayo Wana wa Israili.
60. Basi wakawafuata lilipo chomoza jua.
61. Na yalipo onana majeshi mawili haya, watu wa Musa wakasema: Hakika sisi bila ya shaka tumepatikana!
62. (Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa!
63. Tulimletea wahyi Musa tukamwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa.
64. Na tukawajongeza hapo wale wengine.
65. Tukawaokoa Musa na walio kuwa pamoja naye wote.
66. Kisha tukawazamisha hao wengine.
67. Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara; lakini wengi wao si katika wenye kuamini.
68. Na kwa hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
69. Na wasomee khabari za Ibrahim.
70. Alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?
222. Wanamshukia kila mzushi mkubwa mwingi wa dhambi.
223. Wanawapelekea yale wanayo yasikia; na wengi wao ni waongo.
224. Na watungaji mashairi ni wapotofu ndio wanawafuata.
225. Je! Huwaoni kwamba wao wanatangatanga katika kila bonde?
226. Na kwamba wao husema wasiyo yatenda?
227. Isipo kuwa wale walio amini, na wakatenda mema, na wakamkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi, na wakajitetea wanapo dhulumiwa. Na wanao dhulumu watakuja jua mgeuko gani watakao geuka.