Al-Qiyamah - QURAN - Harun Yahya
-
1. Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!
-
2. Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!
-
3. Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?
-
4. Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!
-
5. Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake.
-
6. Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?
-
7. Basi jicho litapo dawaa,
-
8. Na mwezi utapo patwa,
-
9. Na likakusanywa jua na mwezi,
-
10. Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio?
-
11. La! Hapana pa kukimbilia!
-
12. Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu.
-
13. Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha.
-
14. Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake.
-
15. Na ingawa atatoa chungu ya udhuru.
-
16. Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.
-
17. Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha.
-
18. Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake.
-
19. Kisha ni juu yetu kuubainisha.
-
20. Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,
-
21. Na mnaacha maisha ya Akhera.
-
22. Zipo nyuso siku hiyo zitao ng`ara,
-
23. Zinamwangallia Mola wao Mlezi.
-
24. Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana.
-
25. Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo.
-
26. La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo,
-
27. Na pakasemwa: Nani wa kumganga?
-
28. Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki;
-
29. Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi,
-
30. Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi!
-
31. Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali.
-
32. Bali alikanusha, na akageuka.
-
33. Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao.
-
34. Ole wako, ole wako!
-
35. Kisha Ole wako, ole wako!
-
36. Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure?
-
37. Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?
-
38. Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.
-
39. Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.
-
40. Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?
SHIRIKI
1
Al-Fatihah
2
Al Baqara
3
Ali `Imran
4
An-Nisa
5
Al-Ma`idah
6
Al-An`am
7
Al-A`raf
8
Al-Anfal
9
At-Tawbah
10
Yunus
11
Hud
12
Yusuf
13
Ar-Ra`d
14
Ibrahim
15
Al-Hijr
16
An-Nahl
17
Al-Isra
18
Al-Kahf
19
Maryam
20
Taha
21
Al-Anbya
22
Al-Haj
23
Al-Mu`minun
24
An-Nur
25
Al-Furqan
26
Ash-Shu`ara
27
An-Naml
28
Al-Qasas
29
Al-`Ankabut
30
Ar-Rum
31
Luqman
32
As-Sajdah
33
Al-Ahzab
34
Saba
35
Faatir
36
Ya-Sin
37
As-Saffat
38
Sad
39
Az-Zumar
40
Ghafir
41
Fussilat
42
sh-Shuraa
43
Az-Zukhruf
44
Ad-Dukhan
45
Al-Jathiyah
46
Al-Ahqaf
47
Muhammad
48
Al-Fath
49
Al-Hujurat
50
Qaf
51
Adh-Dhariyat
52
At-Tur
53
An-Najm
54
Al-Qamar
55
Ar-Rahman
56
Al-Waqi`ah
57
Al-Hadid
58
Al-Mujadila
59
Al-Hashr
60
Al-Mumtahanah
61
As-Saf
62
Al-Jumu`ah
63
Al-Munafiqun
64
At-Taghabun
65
At-Talaq
66
At-Tahrim
67
Al-Mulk
68
Al-Qalam
69
Al-Haqqah
70
Al-Ma`arij
71
Nuh
72
Al-Jinn
73
Al-Muzzammil
74
Al-Muddaththir
75
Al-Qiyamah
76
Al-Insan
77
Al-Mursalat
78
An-Naba
79
An-Nazi`at
80
Abasa
81
At-Takwir
82
Al-Infitar
83
Al-Mutaffifin
84
Al-Inshiqaq
85
Al-Buruj
86
At-Tariq
87
Al-A`la
88
Al-Ghashiyah
89
Al-Fajr
90
Al-Balad
91
Ash-Shams
92
Al-Layl
93
Ad-Duhaa
94
Ash-Sharh
95
At-Tin
96
Al-`Alaq
97
Al-Qadr
98
Al-Bayyinah
99
Az-Zalzalah
100
Al-`Adiyat
101
Al-Qari`ah
102
At-Takathur
103
Al-`Asr
104
Al-Humazah
105
Al-Fil
106
Quraysh
107
Al-Ma`un
108
Al-Kawthar
109
Al-Kafirun
110
An-Nasr
111
Al-Masad
112
Al-Ikhlas
113
Al-Falaq
114
An-Nas