logo HARUN YAHYA

Al-Qiyamah - QURAN - Harun Yahya

  • 1. Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!
  • 2. Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!
  • 3. Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?
  • 4. Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!
  • 5. Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake.
  • 6. Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?
  • 7. Basi jicho litapo dawaa,
  • 8. Na mwezi utapo patwa,
  • 9. Na likakusanywa jua na mwezi,
  • 10. Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio?
  • 11. La! Hapana pa kukimbilia!
  • 12. Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu.
  • 13. Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha.
  • 14. Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake.
  • 15. Na ingawa atatoa chungu ya udhuru.
  • 16. Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.
  • 17. Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha.
  • 18. Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake.
  • 19. Kisha ni juu yetu kuubainisha.
  • 20. Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,
  • 21. Na mnaacha maisha ya Akhera.
  • 22. Zipo nyuso siku hiyo zitao ng`ara,
  • 23. Zinamwangallia Mola wao Mlezi.
  • 24. Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana.
  • 25. Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo.
  • 26. La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo,
  • 27. Na pakasemwa: Nani wa kumganga?
  • 28. Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki;
  • 29. Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi,
  • 30. Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi!
  • 31. Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali.
  • 32. Bali alikanusha, na akageuka.
  • 33. Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao.
  • 34. Ole wako, ole wako!
  • 35. Kisha Ole wako, ole wako!
  • 36. Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure?
  • 37. Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?
  • 38. Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.
  • 39. Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.
  • 40. Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?
SHIRIKI
Facebook
X
WhatsApp
Telegram
QR Code
QR Code