75. Al-Qiyamah - Qurani
- 1. Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!
- 2. Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!
- 3. Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?
- 4. Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!
- 5. Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake.
- 6. Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?
- 7. Basi jicho litapo dawaa,
- 8. Na mwezi utapo patwa,
- 9. Na likakusanywa jua na mwezi,