53. An-Najm - Qurani
- 1. Naapa kwa nyota inapo tua,
- 2. Mwenzenu huyu hakupotea, wala hakukosea.
- 3. Wala hatamki kwa matamanio.
- 4. Hayakuwa haya ila ni ufunuo ulio funuliwa;
- 5. Amemfundisha aliye mwingi wa nguvu,
- 6. Mwenye kutua, akatulia,
- 7. Naye yuko juu kabisa upeo wa macho.
- 8. Kisha akakaribia na akateremka.
- 9. Akawa ni kama baina ya mipinde miwili, au karibu zaidi.
- 10. Akamfunulia mja wake (Mwenyezi Mungu) alicho mfunulia.