An-Najm - QURAN - Harun Yahya
-
1. Naapa kwa nyota inapo tua,
-
2. Mwenzenu huyu hakupotea, wala hakukosea.
-
3. Wala hatamki kwa matamanio.
-
4. Hayakuwa haya ila ni ufunuo ulio funuliwa;
-
5. Amemfundisha aliye mwingi wa nguvu,
-
6. Mwenye kutua, akatulia,
-
7. Naye yuko juu kabisa upeo wa macho.
-
8. Kisha akakaribia na akateremka.
-
9. Akawa ni kama baina ya mipinde miwili, au karibu zaidi.
-
10. Akamfunulia mja wake (Mwenyezi Mungu) alicho mfunulia.
-
11. Moyo haukusema uwongo uliyo yaona.
-
12. Je! Mnabishana naye kwa aliyo yaona?
-
13. Na akamwona mara nyingine,
-
14. Penye Mkunazi wa mwisho.
-
15. Karibu yake ndiyo ipo Bustani inayo kaliwa.
-
16. Kilipo ufunika huo Mkunazi hicho kilicho ufunuika.
-
17. Jicho halikuhangaika wala halikuruka mpaka.
-
18. Kwa yakini aliona katika Ishara kubwa kabisa za Mola wake Mlezi.
-
19. Je! Mmemuona Lata na Uzza?
-
20. Na Manaat, mwingine wa tatu?
-
21. Je! Nyinyi mnao wana wanaume na Yeye ndio awe na wanawake?
-
22. Huo ni mgawanyo wa dhulma!
-
23. Hayo hayakuwa ila ni majina mliyo wapa nyinyi na baba zenu. Mwenyezi Mungu hakuleta uthibitisho wowote juu ya hayo. Hawafuati ila dhana tu na kipendacho nafsi. Na kwa yakini uwongofu ulikwisha wafikia kutoka kwa Mola wao Mlezi.
-
24. Ati mtu anakipata kila anacho kitamani?
-
25. Mwenyezi Mungu tu ndiye Mwenye dunia na Akhera.
-
26. Na wako Malaika wangapi mbinguni, ambao uombezi wao hautafaa chochote isipo kuwa baada ya Mwenyezi Mungu kutoa idhini kwa amtakaye na kumridhia.
-
27. Hakika wasio amini Akhera bila ya shaka wao ndio wanawaita Malaika kwa majina ya kike.
-
28. Nao hawana ujuzi wowote kwa hayo isipo kuwa wanafuata dhana tu. Na dhana haisaidii chochote mbele ya haki.
-
29. Basi mwachilie mbali anaye upa kisogo ukumbusho wetu, na wala hataki ila maisha ya dunia.
-
30. Huo ndio mwisho wao wa ujuzi. Hakika Mola wako Mlezi ndiye anaye mjua zaidi mwenye kuipotea njia yake, na Yeye ndiye anaye mjua zaidi mwenye kuongoka.
-
31. Ni vya Mwenyezi Mungu vyote viliomo mbinguni na viliomo katika ardhi, ili awalipe walio tenda ubaya kwa waliyo yatenda, na walio tenda mema awalipe mema.
-
32. Ambao wanajiepusha na madhambi makuu na vitendo vichafu, isipo kuwa makosa khafifu. Hakika Mola wako Mlezi ni Mkunjufu wa maghfira, naye anakujueni sana tangu alipo kuumbeni kutoka kwenye ardhi, na mlipo kuwa mimba matumboni mwa mama zenu. Basi msijisifu usafi. Yeye anamjua sana mwenye kujikinga na maovu.
-
33. Je! Umemwona yule aliye geuka?
-
34. Na akatoa kidogo, kisha akajizuia?
-
35. Je! Anayo huyo ilimu ya ghaibu, basi ndio anaona?
-
36. Au hakuambiwa yaliyomo katika Vitabu vya Musa?
-
37. Na vya Ibrahimu aliye timiza ahadi?
-
38. Ya kwamba hakika nafsi iliyo beba madhambi haibebi madhambi ya mwengine?
-
39. Na ya kwamba hatapata mtu ila aliyo yafanya mwenyewe?
-
40. Na kwamba vitendo vyake vitaonekana?
-
41. Kisha ndio atalipwa malipo yake kwa ukamilifu.
-
42. Na kwamba kwao Mola wako Mlezi ndio mwisho.
-
43. Na kwamba Yeye ndiye anaye leta kicheko na kilio.
-
44. Na kwamba Yeye ndiye anaye fisha na kuhuisha.
-
45. Na kwamba Yeye ndiye aliye umba jozi, dume na jike
-
46. Kutokana na mbegu ya uzazi inapo miminwa.
-
47. Na kwamba ni juu yake ufufuo mwengine.
-
48. Na kwamba ni Yeye ndiye anaye tosheleza na kukinaisha.
-
49. Na kwamba hakika Yeye ndiye Mola Mlezi wa nyota ya Shii`ra.
-
50. Na kwamba Yeye ndiye aliye waangamiza A`di wa kwanza,
-
51. Na Thamudi hakuwabakisha,
-
52. Na kabla yao kaumu ya Nuhu. Na hao hakika walikuwa ni madhaalimu zaidi, na waovu zaidi;
-
53. Na miji iliyo pinduliwa, ni Yeye aliye ipindua.
-
54. Vikaifunika vilivyo funika.
-
55. Basi neema gani ya Mola wako Mlezi unayo ifanyia shaka?
-
56. Hili ni Onyo katika maonyo yale yale ya zamani.
-
57. Kiyama kimekaribia!
-
58. Hapana wa kukifichua isipo kuwa Mwenyezi Mungu.
-
59. Je! Mnayastaajabia maneno haya?
-
60. Na mnacheka, wala hamlii?
-
61. Nanyi mmeghafilika?
-
62. Basi msujudieni Mwenyezi Mungu, na mumuabudu.
SHIRIKI
1
Al-Fatihah
2
Al Baqara
3
Ali `Imran
4
An-Nisa
5
Al-Ma`idah
6
Al-An`am
7
Al-A`raf
8
Al-Anfal
9
At-Tawbah
10
Yunus
11
Hud
12
Yusuf
13
Ar-Ra`d
14
Ibrahim
15
Al-Hijr
16
An-Nahl
17
Al-Isra
18
Al-Kahf
19
Maryam
20
Taha
21
Al-Anbya
22
Al-Haj
23
Al-Mu`minun
24
An-Nur
25
Al-Furqan
26
Ash-Shu`ara
27
An-Naml
28
Al-Qasas
29
Al-`Ankabut
30
Ar-Rum
31
Luqman
32
As-Sajdah
33
Al-Ahzab
34
Saba
35
Faatir
36
Ya-Sin
37
As-Saffat
38
Sad
39
Az-Zumar
40
Ghafir
41
Fussilat
42
sh-Shuraa
43
Az-Zukhruf
44
Ad-Dukhan
45
Al-Jathiyah
46
Al-Ahqaf
47
Muhammad
48
Al-Fath
49
Al-Hujurat
50
Qaf
51
Adh-Dhariyat
52
At-Tur
53
An-Najm
54
Al-Qamar
55
Ar-Rahman
56
Al-Waqi`ah
57
Al-Hadid
58
Al-Mujadila
59
Al-Hashr
60
Al-Mumtahanah
61
As-Saf
62
Al-Jumu`ah
63
Al-Munafiqun
64
At-Taghabun
65
At-Talaq
66
At-Tahrim
67
Al-Mulk
68
Al-Qalam
69
Al-Haqqah
70
Al-Ma`arij
71
Nuh
72
Al-Jinn
73
Al-Muzzammil
74
Al-Muddaththir
75
Al-Qiyamah
76
Al-Insan
77
Al-Mursalat
78
An-Naba
79
An-Nazi`at
80
Abasa
81
At-Takwir
82
Al-Infitar
83
Al-Mutaffifin
84
Al-Inshiqaq
85
Al-Buruj
86
At-Tariq
87
Al-A`la
88
Al-Ghashiyah
89
Al-Fajr
90
Al-Balad
91
Ash-Shams
92
Al-Layl
93
Ad-Duhaa
94
Ash-Sharh
95
At-Tin
96
Al-`Alaq
97
Al-Qadr
98
Al-Bayyinah
99
Az-Zalzalah
100
Al-`Adiyat
101
Al-Qari`ah
102
At-Takathur
103
Al-`Asr
104
Al-Humazah
105
Al-Fil
106
Quraysh
107
Al-Ma`un
108
Al-Kawthar
109
Al-Kafirun
110
An-Nasr
111
Al-Masad
112
Al-Ikhlas
113
Al-Falaq
114
An-Nas