HARUN YAHYA
Swahili / Kiswahili
SW
QURAN
Al-Qamar
1. Saa imekaribia, na mwezi umepasuka!
2. Na wakiona Ishara hugeuka upande na husema: Huu uchawi tu unazidi kuendelea.
3. Na wamekanusha na wamefuata matamanio yao. Na kila jambo ni lenye kuthibiti.
4. Na bila ya shaka zimewajia khabari zenye makaripio.
5. Hikima kaamili; lakini maonyo hayafai kitu!
6. Basi jiepushe nao. Siku atakapo ita mwitaji kuliendea jambo linalo chusha;
7. Macho yao yatainama; watatoka makaburini kama nzige walio tawanyika,
8. Wanamkimbilia mwitaji, na makafiri wanasema: Hii ni siku ngumu.
9. Kabla yao kaumu ya Nuhu walikanusha; wakamkanusha mja wetu, na wakasema ni mwendawazimu, na akakaripiwa.
10. Basi akamwomba Mola wake Mlezi akasema: Kwa hakika mimi nimeshindwa, basi ninusuru!
11. Basi tukaifungua milango ya mbingu kwa maji yanayo miminika.
12. Na tukazipasua ardhi kwa chemchem, yakakutana maji kwa jambo lilio kadiriwa.
13. Na tukamchukua kwenye safina ya mbao na kamba.
14. Ikawa inakwenda kwa nadhari yetu, kuwa ni malipo kwa alivyo kuwa amekanushwa.
15. Na bila ya shaka tuliiacha iwe ni Ishara. Lakini je, yupo anaye kumbuka?
16. Basi ilikuwaje adhabu yangu, na maonyo yangu.
17. Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur`ani iwe nyepesi kufahamika. Lakini yupo anaye kumbuka?
18. Kina A`di walikanusha. Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?
19. Hakika Sisi tuliwapelekea upepo wa kimbunga katika siku korofi mfululizo,
20. Ukiwang`oa watu kama vigogo vya mitende vilio ng`olewa.
21. Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?
22. Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur`ani nyepesi kufahamika; lakini yupo anaye kumbuka?
23. Thamudi waliwakanusha Waonyaji.
24. Wakasema: Ati tumfuate binaadamu mmoja katika sisi? Basi hivyo sisi tutakuwa katika upotofu na kichaa!
25. Ni yeye tu aliye teremshiwa huo ukumbusho kati yetu sote? Bali huyu ni mwongo mwenye kiburi!
26. Kesho watajua ni nani huyo mwongo mwenye kiburi.
27. Hakika Sisi tutawapelekea ngamia jike ili kuwajaribu, basi watazame tu na ustahamili.
28. Na waambie kwamba maji yatagawanywa baina yao; kila sehemu ya maji itahudhuriwa na aliye khusika.
29. Basi wakamwita mtu wao akaja akamchinja.
30. Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu!
31. Hakika Sisi tuliwapelekea ukelele mmoja tu, wakawa kama mabuwa ya kujengea uwa.
32. Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur`ani iwe nyepesi kwa kukumbuka, lakini yupo akumbukaye?
33. Kaumu Lut`i nao waliwakadhibisha Waonyaji.
34. Hakika Sisi tukawapelekea kimbunga cha vijiwe, isipo kuwa wafuasi wa Lut`i. Hao tuliwaokoa karibu na alfajiri.
35. Kwa neema inayo toka kwetu. Hivyo ndivyo tumlipavyo anaye shukuru.
36. Na hakika yeye aliwaonya adhabu yetu; lakini wao waliyatilia shaka hayo maonyo.
37. Na walimtaka awape wageni wake. Tukayapofua macho yao, na tukawaambia: Onjeni basi adhabu na maonyo yangu!
38. Na iliwafikia wakati wa asubuhi adhabu yangu ya kuendelea.
39. Basi onjeni adhabu na maonyo yangu!
40. Na hakika tumeisahilisha Qur`ani kuikumbuka. Lakini yupo anaye kumbuka?
41. Na Waonyaji waliwafikia watu wa Firauni.
42. Walizikadhibisha Ishara zetu zote, nasi tukawashika kama anavyo shika Mwenye nguvu Mwenye uweza.
43. Je! Makafiri wenu ni bora kuliko hao, au yameandikwa vitabuni kuwa nyinyi hamtiwi makosani?
44. Au ndio wanasema: Sisi ni wengi tutashinda tu.
45. Wingi wao huu utashindwa, na wao watasukumwa nyuma.
46. Bali Saa ya Kiyama ndio miadi yao, na Saa hiyo ni nzito zaidi na chungu zaidi.
47. Hakika wakosefu wamo katika upotofu na wazimu.
48. Siku watakapo kokotwa Motoni kifudifudi waambiwe: Onjeni mguso wa Jahannamu!
49. Kwa hakika Sisi tumekiumba kila kitu kwa kipimo.
50. Na amri yetu haikuwa ila ni moja tu, kama kupepesa jicho.
51. Na bila ya shaka tumekwisha waangamiza wenzenu. Lakini yupo anaye kumbuka?
52. Na kila jambo walilo lifanya limo vitabuni.
53. Na kila kidogo na kikubwa kimeandikwa.
54. Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na mito.
55. Katika makalio ya haki kwa Mfalme Mwenye uweza.
SHIRIKI
1. Al-Fatihah
2. Al Baqara
3. Ali `Imran
4. An-Nisa
5. Al-Ma`idah
6. Al-An`am
7. Al-A`raf
8. Al-Anfal
9. At-Tawbah
10. Yunus
11. Hud
12. Yusuf
13. Ar-Ra`d
14. Ibrahim
15. Al-Hijr
16. An-Nahl
17. Al-Isra
18. Al-Kahf
19. Maryam
20. Taha
21. Al-Anbya
22. Al-Haj
23. Al-Mu`minun
24. An-Nur
25. Al-Furqan
26. Ash-Shu`ara
27. An-Naml
28. Al-Qasas
29. Al-`Ankabut
30. Ar-Rum
31. Luqman
32. As-Sajdah
33. Al-Ahzab
34. Saba
35. Faatir
36. Ya-Sin
37. As-Saffat
38. Sad
39. Az-Zumar
40. Ghafir
41. Fussilat
42. sh-Shuraa
43. Az-Zukhruf
44. Ad-Dukhan
45. Al-Jathiyah
46. Al-Ahqaf
47. Muhammad
48. Al-Fath
49. Al-Hujurat
50. Qaf
51. Adh-Dhariyat
52. At-Tur
53. An-Najm
54. Al-Qamar
55. Ar-Rahman
56. Al-Waqi`ah
57. Al-Hadid
58. Al-Mujadila
59. Al-Hashr
60. Al-Mumtahanah
61. As-Saf
62. Al-Jumu`ah
63. Al-Munafiqun
64. At-Taghabun
65. At-Talaq
66. At-Tahrim
67. Al-Mulk
68. Al-Qalam
69. Al-Haqqah
70. Al-Ma`arij
71. Nuh
72. Al-Jinn
73. Al-Muzzammil
74. Al-Muddaththir
75. Al-Qiyamah
76. Al-Insan
77. Al-Mursalat
78. An-Naba
79. An-Nazi`at
80. Abasa
81. At-Takwir
82. Al-Infitar
83. Al-Mutaffifin
84. Al-Inshiqaq
85. Al-Buruj
86. At-Tariq
87. Al-A`la
88. Al-Ghashiyah
89. Al-Fajr
90. Al-Balad
91. Ash-Shams
92. Al-Layl
93. Ad-Duhaa
94. Ash-Sharh
95. At-Tin
96. Al-`Alaq
97. Al-Qadr
98. Al-Bayyinah
99. Az-Zalzalah
100. Al-`Adiyat
101. Al-Qari`ah
102. At-Takathur
103. Al-`Asr
104. Al-Humazah
105. Al-Fil
106. Quraysh
107. Al-Ma`un
108. Al-Kawthar
109. Al-Kafirun
110. An-Nasr
111. Al-Masad
112. Al-Ikhlas
113. Al-Falaq
114. An-Nas