1. Al-Fatihah - Qurani
- 1. KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.
- 2. Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote;
- 3. Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu;
- 4. Mwenye Kumiliki Siku ya Malipo.
- 5. Wewe tu tunakuabudu, na Wewe tu tunakuomba msaada.
- 6. Tuongoe njia iliyo nyooka,
- 7. Njia ya ulio waneemesha, siyo ya walio kasirikiwa, wala walio potea.