86. At-Tariq - Qurani
- 1. Naapa kwa mbingu na Kinacho kuja usiku!
- 2. Na nini kitakacho kujuulisha ni nini hicho Kinacho kuja usiku?
- 3. Ni Nyota yenye mwanga mkali.
- 4. Hapana nafsi ila inayo mwangalizi.
- 5. Hebu naajitazame mwanaadamu ameumbwa kwa kitu gani?
- 6. Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa,
- 7. Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu.
- 8. Hakika Yeye ana uweza wa kumrudisha.
- 9. Siku zitakapo dhihirishwa siri.