• 1. Naapa kwa mbingu na Kinacho kuja usiku!

  • 2. Na nini kitakacho kujuulisha ni nini hicho Kinacho kuja usiku?

  • 3. Ni Nyota yenye mwanga mkali.

  • 4. Hapana nafsi ila inayo mwangalizi.

  • 5. Hebu naajitazame mwanaadamu ameumbwa kwa kitu gani?

  • 6. Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa,

  • 7. Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu.

  • 8. Hakika Yeye ana uweza wa kumrudisha.

  • 9. Siku zitakapo dhihirishwa siri.

  • 10. Basi hatakuwa na nguvu wala msaidizi.

  • 11. Naapa kwa mbingu yenye marejeo!

  • 12. Na kwa ardhi inayo pasuka!

  • 13. Hakika hii ni kauli ya kupambanua.

  • 14. Wala si mzaha.

  • 15. Hakika wao wanapanga mpango.

  • 16. Na Mimi napanga mpango.

  • 17. Basi wape muhula makafiri - wape muhula pole pole.