99. Az-Zalzalah - Qurani
- 1. Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake!
- 2. Na itakapo toa ardhi mizigo yake!
- 3. Na mtu akasema: Ina nini?
- 4. Siku hiyo itahadithia khabari zake.
- 5. Kwa sababu Mola wake Mlezi ameifunulia!
- 6. Siku hiyo watu watatoka kwa mfarakano wakaonyweshwe vitendo vyao!
- 7. Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona!
- 8. Na anaye tenda chembe ya uovu atauona!