Ad-Dukhan - QURAN - Harun Yahya
-
1. H`a Mim
-
2. Naapa kwa Kitabu kinacho bainisha,
-
3. Hakika tumekiteremsha katika usiku ulio barikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji.
-
4. Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hikima,
-
5. Jambo litokalo kwetu. Hakika Sisi ndio wenye kutuma.
-
6. Ni rehema itokayo kwa Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia Mwenye kujua.
-
7. Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, ikiwa nyinyi mna yakini.
-
8. Hakuna mungu ila Yeye; anahuisha na anafisha- Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa mwanzo.
-
9. Lakini wao wanacheza katika shaka.
-
10. Basi ingoje siku ambayo mbingu zitakapo leta moshi ulio dhaahiri,
-
11. Utakao wafunika watu: Hii ni adhabu chungu!
-
12. Mola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu hii. Hakika tutaamini.
-
13. Nini faida ya kukumbuka kwao? Na alikwisha wafikia Mtume mwenye kubainisha.
-
14. Na wao wakamgeuzia uso, na wakasema: Huyu amefunzwa, naye ni mwendawazimu.
-
15. Hakika sisi tutaiondoa adhabu kidogo, lakini nyinyi kwa yakini mtarejea vile vile!
-
16. Siku tutayo yashambulia mashambulio makubwa, bila ya shaka Sisi ni wenye kutesa.
-
17. Na hakika kabla ya hawa tuliwafanyia mtihani watu wa Firauni, na aliwafikia Mtume Mtukufu.
-
18. Akasema: Nipeni waja wa Mwenyezi Mungu; kwa hakika mimi kwenu ni Mtume Muaminifu.
-
19. Na msimfanyie kiburi Mwenyezi Mungu; hakika mimi nitakuleteeni uthibitisho ulio wazi.
-
20. Nami najikinga kwa Mola wangu Mlezi na ndiye Mola wenu Mlezi pia, ili msinipige mawe.
-
21. Na ikiwa hamniamini, basi jitengeni nami.
-
22. Ndipo akamwomba Mola wake Mlezi: Hakika watu hawa ni wakosefu.
-
23. Mwenyezi Mungu akasema: Basi nenda na waja wangu usiku. Kwa yakini mtafuatwa.
-
24. Na iache bahari vivyo hivyo imeachana, hakika wao hao ni jeshi litakalo zamishwa.
-
25. Mabustani mangapi, na chemchem ngapi waliziacha!
-
26. Na mimea na vyeo vitukufu!
-
27. Na neema walizo kuwa wakijistareheshea!
-
28. Ndio hivyo! Na tukawarithisha haya watu wenginewe.
-
29. La mbingu wala ardhi hazikuwalilia, wala hawakupewa muhula.
-
30. Na bila ya shaka tuliwaokoa Wana wa Israili katika adhabu ya kuwadhalilisha,
-
31. Ya Firauni. Hakika yeye alikuwa jeuri katika wenye kupindukia mipaka.
-
32. Na tuliwakhiari kwa ujuzi wetu kuliko walimwengu wenginewe.
-
33. Na tukawapa katika ishara zenye majaribio yaliyo wazi.
-
34. Hakika hawa wanasema:
-
35. Hapana ila kufa kwetu mara ya kwanza tu, wala sisi hatufufuliwi.
-
36. Basi warudisheni baba zetu, ikiwa nyinyi mnasema kweli.
-
37. Je! Ni wao bora au watu wa Tubbaa` na walio kuwa kabla yao? Tuliwaangamiza. Hakika hao walikuwa wakosefu.
-
38. Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake kwa mchezo.
-
39. Hatukuviumba hivyo ila kwa Haki, lakini wengi wao hawajui.
-
40. Hakika siku ya Uamuzi ni wakati ulio wekwa kwa wao wote.
-
41. Siku ambayo rafiki hatamfaa rafiki yake kwa chochote, wala hawatanusuriwa.
-
42. Isipo kuwa atakaye mrehemu Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
-
43. Hakika Mti wa Zaqqum,
-
44. Ni chakula cha mwenye dhambi.
-
45. Kama shaba iliyo yayushwa, hutokota matumboni
-
46. Kama kutokota kwa maji ya moto.
-
47. (Itasemwa:) Mkamateni na mtupeni katikati ya Jahannamu!
-
48. Kisha mmwagieni juu ya kichwa chake adhabu ya maji yanayo chemka.
-
49. Onja! Ati wewe ndiye mwenye nguvu, mtukufu!
-
50. Hakika haya ndiyo mliyo kuwa mkiyatilia shaka.
-
51. Hakika wachamngu watakuwa katika mahali pa amani,
-
52. Katika mabustani na chemchem,
-
53. Watavaa hariri nyepesi na hariri nzito wakikabiliana,
-
54. Hivi ndivyo itakavyo kuwa, na tutawaoza mahurilaini.
-
55. Humo watataka kila aina ya matunda, na wakae kwa amani.
-
56. Humo hawataonja mauti ila mauti yale ya kwanza, na (Mwenyezi Mungu) atawalinda na adhabu ya Jahannamu,
-
57. Kuwa ni fadhila zitokazo kwa Mola wako Mlezi. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
-
58. Basi tumeifanya nyepesi hii Qur`ani kwa ulimi wako, ili wapate kukumbuka.
-
59. Ngoja tu, na wao wangoje pia.
SHIRIKI
1
Al-Fatihah
2
Al Baqara
3
Ali `Imran
4
An-Nisa
5
Al-Ma`idah
6
Al-An`am
7
Al-A`raf
8
Al-Anfal
9
At-Tawbah
10
Yunus
11
Hud
12
Yusuf
13
Ar-Ra`d
14
Ibrahim
15
Al-Hijr
16
An-Nahl
17
Al-Isra
18
Al-Kahf
19
Maryam
20
Taha
21
Al-Anbya
22
Al-Haj
23
Al-Mu`minun
24
An-Nur
25
Al-Furqan
26
Ash-Shu`ara
27
An-Naml
28
Al-Qasas
29
Al-`Ankabut
30
Ar-Rum
31
Luqman
32
As-Sajdah
33
Al-Ahzab
34
Saba
35
Faatir
36
Ya-Sin
37
As-Saffat
38
Sad
39
Az-Zumar
40
Ghafir
41
Fussilat
42
sh-Shuraa
43
Az-Zukhruf
44
Ad-Dukhan
45
Al-Jathiyah
46
Al-Ahqaf
47
Muhammad
48
Al-Fath
49
Al-Hujurat
50
Qaf
51
Adh-Dhariyat
52
At-Tur
53
An-Najm
54
Al-Qamar
55
Ar-Rahman
56
Al-Waqi`ah
57
Al-Hadid
58
Al-Mujadila
59
Al-Hashr
60
Al-Mumtahanah
61
As-Saf
62
Al-Jumu`ah
63
Al-Munafiqun
64
At-Taghabun
65
At-Talaq
66
At-Tahrim
67
Al-Mulk
68
Al-Qalam
69
Al-Haqqah
70
Al-Ma`arij
71
Nuh
72
Al-Jinn
73
Al-Muzzammil
74
Al-Muddaththir
75
Al-Qiyamah
76
Al-Insan
77
Al-Mursalat
78
An-Naba
79
An-Nazi`at
80
Abasa
81
At-Takwir
82
Al-Infitar
83
Al-Mutaffifin
84
Al-Inshiqaq
85
Al-Buruj
86
At-Tariq
87
Al-A`la
88
Al-Ghashiyah
89
Al-Fajr
90
Al-Balad
91
Ash-Shams
92
Al-Layl
93
Ad-Duhaa
94
Ash-Sharh
95
At-Tin
96
Al-`Alaq
97
Al-Qadr
98
Al-Bayyinah
99
Az-Zalzalah
100
Al-`Adiyat
101
Al-Qari`ah
102
At-Takathur
103
Al-`Asr
104
Al-Humazah
105
Al-Fil
106
Quraysh
107
Al-Ma`un
108
Al-Kawthar
109
Al-Kafirun
110
An-Nasr
111
Al-Masad
112
Al-Ikhlas
113
Al-Falaq
114
An-Nas