88. Al-Ghashiyah - Qurani
- 1. Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?
- 2. Siku hiyo nyuso zitainama,
- 3. Zikifanya kazi, nazo taabani.
- 4. Ziingie katika Moto unao waka -
- 5. Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.
- 6. Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.
- 7. Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.
- 8. Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.
- 9. Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,