80. Abasa - Qurani
- 1. Alikunja kipaji na akageuka,
- 2. Kwa sababu alimjia kipofu!
- 3. Na nini kitakujuulisha pengine yeye atatakasika?
- 4. Au atawaidhika, na mawaidha yamfae?
- 5. Ama ajionaye hana haja,
- 6. Wewe ndio unamshughulikia?
- 7. Na si juu yako kama hakutakasika.
- 8. Ama anaye kujia kwa juhudi,
- 9. Naye anaogopa,
- 10. Ndio wewe unampuuza?