logo HARUN YAHYA

Al-Fajr - QURAN - Harun Yahya

  • 1. Naapa kwa alfajiri,
  • 2. Na kwa masiku kumi,
  • 3. Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,
  • 4. Na kwa usiku unapo pita,
  • 5. Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?
  • 6. Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A`di?
  • 7. Wa Iram, wenye majumba marefu?
  • 8. Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?
  • 9. Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?
  • 10. Na Firauni mwenye vigingi?
  • 11. Ambao walifanya jeuri katika nchi?
  • 12. Wakakithirisha humo ufisadi?
  • 13. Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu.
  • 14. Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia.
  • 15. Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu!
  • 16. Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!
  • 17. Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,
  • 18. Wala hamhimizani kulisha masikini;
  • 19. Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,
  • 20. Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi.
  • 21. Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,
  • 22. Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,
  • 23. Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?
  • 24. Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu!
  • 25. Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.
  • 26. Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake.
  • 27. Ewe nafsi iliyo tua!
  • 28. Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.
  • 29. Basi ingia miongoni mwa waja wangu,
  • 30. Na ingia katika Pepo yangu.
SHIRIKI
Facebook
X
WhatsApp
Telegram
QR Code
QR Code