89. Al-Fajr - Qurani
- 1. Naapa kwa alfajiri,
- 2. Na kwa masiku kumi,
- 3. Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,
- 4. Na kwa usiku unapo pita,
- 5. Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?
- 6. Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A`di?
- 7. Wa Iram, wenye majumba marefu?
- 8. Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?
- 9. Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?