Al-Ma`arij - QURAN - Harun Yahya
-
1. Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea,
-
2. Kwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia -
-
3. Kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja.
-
4. Malaika na Roho hupanda kwendea kwake katika siku ambayo kadiri yake ni miaka khamsini elfu!
-
5. Basi subiri kwa subira njema.
-
6. Hakika wao wanaiona iko mbali,
-
7. Na Sisi tunaiona iko karibu.
-
8. Siku ambayo mbingu zitakapo kuwa kama maadeni iliyo yayushwa.
-
9. Na milima itakuwa kama sufi.
-
10. Wala jamaa hatamuuliza jamaa yake.
-
11. Ijapo kuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe,
-
12. Na mkewe, na nduguye,
-
13. Na jamaa zake walio kuwa wakimkimu,
-
14. Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye.
-
15. La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa,
-
16. Unao babua ngozi ya kichwa!
-
17. Utamwita kila aliye geuza mgongo na akageuka.
-
18. Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi.
-
19. Hakika mtu ameumbwa na papara.
-
20. Inapo mgusa shari hupapatika.
-
21. Na inapo mgusa kheri huizuilia.
-
22. Isipo kuwa wanao sali,
-
23. Ambao wanadumisha Sala zao,
-
24. Na ambao katika mali yao iko haki maalumu
-
25. Kwa mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba;
-
26. Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo,
-
27. Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi.
-
28. Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo.
-
29. Na ambao wanahifadhi tupu zao.
-
30. Isipo kuwa kwa wake zao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi -
-
31. Lakini wanao taka kinyume ya haya, basi hao ndio wanao ruka mipaka.
-
32. Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao,
-
33. Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao,
-
34. Na ambao wanazihifadhi Sala zao.
-
35. Hao ndio watakao hishimiwa Peponi.
-
36. Wana nini wale walio kufuru wanakutumbulia macho tu?
-
37. Makundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto!
-
38. Kwani kila mmoja wao anatumai kuingizwa katika Pepo ya neema?
-
39. La, hasha! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na wanacho kijua.
-
40. Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mashariki zote na magharibi zote kwamba Sisi tunaweza
-
41. Kuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi.
-
42. Basi waache wapige porojo na wacheze, mpaka wakutane na siku yao wanayo ahidiwa,
-
43. Siku watakapotoka makaburini kwa upesi kama kwamba wanakimbilia mfundo,
-
44. Macho yao yatainama, fedheha itawafunika. Hiyo ndiyo Siku waliyo kuwa wakiahidiwa.
SHIRIKI
1
Al-Fatihah
2
Al Baqara
3
Ali `Imran
4
An-Nisa
5
Al-Ma`idah
6
Al-An`am
7
Al-A`raf
8
Al-Anfal
9
At-Tawbah
10
Yunus
11
Hud
12
Yusuf
13
Ar-Ra`d
14
Ibrahim
15
Al-Hijr
16
An-Nahl
17
Al-Isra
18
Al-Kahf
19
Maryam
20
Taha
21
Al-Anbya
22
Al-Haj
23
Al-Mu`minun
24
An-Nur
25
Al-Furqan
26
Ash-Shu`ara
27
An-Naml
28
Al-Qasas
29
Al-`Ankabut
30
Ar-Rum
31
Luqman
32
As-Sajdah
33
Al-Ahzab
34
Saba
35
Faatir
36
Ya-Sin
37
As-Saffat
38
Sad
39
Az-Zumar
40
Ghafir
41
Fussilat
42
sh-Shuraa
43
Az-Zukhruf
44
Ad-Dukhan
45
Al-Jathiyah
46
Al-Ahqaf
47
Muhammad
48
Al-Fath
49
Al-Hujurat
50
Qaf
51
Adh-Dhariyat
52
At-Tur
53
An-Najm
54
Al-Qamar
55
Ar-Rahman
56
Al-Waqi`ah
57
Al-Hadid
58
Al-Mujadila
59
Al-Hashr
60
Al-Mumtahanah
61
As-Saf
62
Al-Jumu`ah
63
Al-Munafiqun
64
At-Taghabun
65
At-Talaq
66
At-Tahrim
67
Al-Mulk
68
Al-Qalam
69
Al-Haqqah
70
Al-Ma`arij
71
Nuh
72
Al-Jinn
73
Al-Muzzammil
74
Al-Muddaththir
75
Al-Qiyamah
76
Al-Insan
77
Al-Mursalat
78
An-Naba
79
An-Nazi`at
80
Abasa
81
At-Takwir
82
Al-Infitar
83
Al-Mutaffifin
84
Al-Inshiqaq
85
Al-Buruj
86
At-Tariq
87
Al-A`la
88
Al-Ghashiyah
89
Al-Fajr
90
Al-Balad
91
Ash-Shams
92
Al-Layl
93
Ad-Duhaa
94
Ash-Sharh
95
At-Tin
96
Al-`Alaq
97
Al-Qadr
98
Al-Bayyinah
99
Az-Zalzalah
100
Al-`Adiyat
101
Al-Qari`ah
102
At-Takathur
103
Al-`Asr
104
Al-Humazah
105
Al-Fil
106
Quraysh
107
Al-Ma`un
108
Al-Kawthar
109
Al-Kafirun
110
An-Nasr
111
Al-Masad
112
Al-Ikhlas
113
Al-Falaq
114
An-Nas