logo HARUN YAHYA

Al-Ma`arij - QURAN - Harun Yahya

  • 1. Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea,
  • 2. Kwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia -
  • 3. Kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja.
  • 4. Malaika na Roho hupanda kwendea kwake katika siku ambayo kadiri yake ni miaka khamsini elfu!
  • 5. Basi subiri kwa subira njema.
  • 6. Hakika wao wanaiona iko mbali,
  • 7. Na Sisi tunaiona iko karibu.
  • 8. Siku ambayo mbingu zitakapo kuwa kama maadeni iliyo yayushwa.
  • 9. Na milima itakuwa kama sufi.
  • 10. Wala jamaa hatamuuliza jamaa yake.
  • 11. Ijapo kuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe,
  • 12. Na mkewe, na nduguye,
  • 13. Na jamaa zake walio kuwa wakimkimu,
  • 14. Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye.
  • 15. La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa,
  • 16. Unao babua ngozi ya kichwa!
  • 17. Utamwita kila aliye geuza mgongo na akageuka.
  • 18. Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi.
  • 19. Hakika mtu ameumbwa na papara.
  • 20. Inapo mgusa shari hupapatika.
  • 21. Na inapo mgusa kheri huizuilia.
  • 22. Isipo kuwa wanao sali,
  • 23. Ambao wanadumisha Sala zao,
  • 24. Na ambao katika mali yao iko haki maalumu
  • 25. Kwa mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba;
  • 26. Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo,
  • 27. Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi.
  • 28. Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo.
  • 29. Na ambao wanahifadhi tupu zao.
  • 30. Isipo kuwa kwa wake zao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi -
  • 31. Lakini wanao taka kinyume ya haya, basi hao ndio wanao ruka mipaka.
  • 32. Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao,
  • 33. Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao,
  • 34. Na ambao wanazihifadhi Sala zao.
  • 35. Hao ndio watakao hishimiwa Peponi.
  • 36. Wana nini wale walio kufuru wanakutumbulia macho tu?
  • 37. Makundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto!
  • 38. Kwani kila mmoja wao anatumai kuingizwa katika Pepo ya neema?
  • 39. La, hasha! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na wanacho kijua.
  • 40. Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mashariki zote na magharibi zote kwamba Sisi tunaweza
  • 41. Kuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi.
  • 42. Basi waache wapige porojo na wacheze, mpaka wakutane na siku yao wanayo ahidiwa,
  • 43. Siku watakapotoka makaburini kwa upesi kama kwamba wanakimbilia mfundo,
  • 44. Macho yao yatainama, fedheha itawafunika. Hiyo ndiyo Siku waliyo kuwa wakiahidiwa.
SHIRIKI
Facebook
X
WhatsApp
Telegram
QR Code
QR Code