92. Al-Layl - Qurani
- 1. Naapa kwa usiku unapo funika!
- 2. Na mchana unapo dhihiri!
- 3. Na kwa Aliye umba dume na jike!
- 4. Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni mbali mbali.
- 5. Ama mwenye kutoa na akamchamngu,
- 6. Na akaliwafiki lilio jema,
- 7. Tutamsahilishia yawe mepesi.
- 8. Na ama mwenye kufanya ubakhili, na asiwe na haja ya wenzake,
- 9. Na akakanusha lilio jema,
- 10. Tutamsahilishia yawe mazito!