82. Al-Infitar - Qurani
- 1. Mbingu itapo chanika,
- 2. Na nyota zitapo tawanyika,
- 3. Na bahari zitakapo pasuliwa,
- 4. Na makaburi yatapo fukuliwa,
- 5. Hapo kila nafsi itajua ilicho tanguliza, na ilicho bakisha nyuma.
- 6. Ewe mwanaadamu! Nini kilicho kughuri ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?
- 7. Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha,
- 8. Katika sura yoyote aliyo ipenda akakujenga.
- 9. Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo.