Ya-Sin - QURAN - Harun Yahya
-
1. Ya-Sin (Y. S.).
-
2. Kwa Haki ya Qur`ani yenye hikima!
-
3. Hakika wewe ni miongoni mwa walio tumwa,
-
4. Juu ya Njia Iliyo Nyooka.
-
5. Uteremsho wa Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
-
6. Ili uwaonye watu ambao baba zao hawakuonywa, basi wao wamekuwa wenye kughafilika.
-
7. Bila ya shaka kauli imekwisha thibiti juu ya wengi katika wao, kwa hivyo hawaamini.
-
8. Tumeweka makongwa shingoni mwao, yakawafika videvuni. Kwa hivyo vichwa vyao viko juu tu.
-
9. Tumeweka kizuizi mbele yao, na kizuizi nyuma yao, na tumewafunika macho yao; kwa hivyo hawaoni.
-
10. Ni sawa sawa kwao ukiwaonya au usiwaonye, hawataamini.
-
11. Hakika wewe unamwonya mwenye kufuata ukumbusho, na akamcha Arrahman, Mwingi wa Rehema, kwa ghaibu. Basi mbashirie huyo msamaha na ujira mwema.
-
12. Hakika Sisi tunawafufua wafu, na tunayaandika wanayo yatanguliza, na wanayo yaacha nyuma. Na kila kitu tumekihifadhi katika daftari asli lenye kubainisha.
-
13. Na wapigie mfano wa wakaazi wa mji walipo wafikia walio tumwa.
-
14. Tulipo watumia wawili, wakawakanusha. Basi tukawazidishia nguvu kwa mwingine wa tatu. Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwenu.
-
15. Wakasema: Nyinyi si chochote ila ni watu kama sisi. Na Mwingi wa Rehema hakuteremsha kitu. Nyinyi mnasema uwongo tu.
-
16. Wakasema: Mola wetu Mlezi anajua kwamba hakika sisi tumetumwa kwenu.
-
17. Wala si juu yetu ila kufikisha ujumbe ulio wazi.
-
18. Wakasema: Sisi tumeagua kuwa nyinyi ni wakorofi. Ikiwa hamtaacha basi kwa yakini tutakupigeni mawe, na mtapata adhabu chungu kutoka kwetu.
-
19. Wakasema: Ukorofi wenu mnao wenyewe! Je! Ni kwa kuwa mnakumbushwa? Ama nyinyi ni watu walio pindukia mipaka.
-
20. Na akaja mtu mbio kutokea upande wa mbali wa mjini, akasema: Enyi watu wangu! Wafuateni hawa walio tumwa.
-
21. Wafuateni ambao hawakutakini ujira, hali ya kuwa wenyewe wameongoka.
-
22. NA KWA NINI nisimuabudu yule aliye niumba na kwake mtarejeshwa?
-
23. Je! Niishike miungu mingine badala yake? Arrahmani, Mwingi wa Rehema, akinitakia madhara uombezi wa hao hautanifaa kitu, wala hawataniokoa.
-
24. Basi hakika mimi hapo nitakuwa katika upotovu ulio dhaahiri.
-
25. Hakika mimi nimemuamini Mola wenu Mlezi, basi nisikilizeni!
-
26. Akaambiwa: Ingia Peponi! Akasema: Laiti kuwa watu wangu wangeli jua
-
27. Jinsi Mola wangu Mlezi alivyo nisamehe, na akanifanya miongoni mwa walio hishimiwa.
-
28. Na hatukuwateremshia kaumu yake baada yake jeshi kutoka mbinguni, wala si wenye kuteremsha.
-
29. Hakukuwa ila ukelele mmoja tu; na mara walizimwa!
-
30. Nawasikitikia waja wangu. Hawajii Mtume ila wao humkejeli.
-
31. Je! Hawaoni umma ngapi tulizo ziangamiza kabla yao? Hakika hao hawarejei tena kwao.
-
32. Na hapana mmoja ila wote watakusanywa waletwe mbele yetu.
-
33. Na Ishara hiyo kwao - ardhi iliyo kufa, nasi tukaifufua, na tukatoa ndani yake nafaka, wakawa wanazila!
-
34. Na tukafanya ndani yake mabustani ya mitende na mizabibu, na tukatimbua chemchem ndani yake,
-
35. Ili wale matunda yake, na hayo hayakufanywa na mikono yao! Basi je, hawashukuru?
-
36. Subhana, Ametakasika, aliye umba dume na jike vyote katika vinavyo mea katika ardhi na katika nafsi zao, na katika wasivyo vijua.
-
37. Na usiku ni Ishara kwao. Tunauvua humo mchana, mara wao wanakuwa gizani.
-
38. Na jua linakwenda kwa kiwango chake. Hayo ni makadirio ya Mwenye nguvu, Mwenye kujua.
-
39. Na mwezi tumeupimia vituo, mpaka unakuwa kama karara kongwe.
-
40. Haliwi jua kuufikia mwezi, wala usiku kuupita mchana. Na vyote vinaogelea katika njia zao.
-
41. Na ni Ishara kwao kwamba Sisi tuliwapakia dhuriya zao katika jahazi ilio sheheni.
-
42. Na tukawaumbia kutoka mfano wake wanavyo vipanda.
-
43. Na tukitaka tunawazamisha, wala hapana wa kuwasaidia, wala hawaokolewi,
-
44. Isipo kuwa kwa rehema zitokazo kwetu na starehe kwa muda.
-
45. Na wanapo ambiwa: Jilindeni na yalioko mbele yenu na yalioko nyuma yenu, ili mpate kurehemewa...
-
46. Na haiwafikii Ishara yoyote katika Ishara za Mola wao Mlezi ila wao huwa ni wenye kuipuuza.
-
47. Na wanapo ambiwa: Toeni katika aliyo kupeni Mwenyezi Mungu, walio kufuru huwaambia walio amini: Je! Tuwalishe ambao Mwenyezi Mungu angependa angeli walisha mwenyewe? Nyinyi hammo ila katika upotofu ulio dhaahiri.
-
48. Na wanasema: Ahadi hii itatokea lini, ikiwa nyinyi ni wakweli?
-
49. Hawangojei ila ukelele mmoja tu utakao wachukua nao wamo kuzozana.
-
50. Basi hawataweza kuusia, wala kwa watu wao hawarejei.
-
51. Na litapulizwa barugumu, mara watatoka makaburini wakikimbilia kwa Mola wao Mlezi.
-
52. Watasema: Ole wetu! Nani aliye tufufua kwenye malazi yetu? Haya ndiyo aliyo yaahidi Mwingi wa Rehema na wakasema kweli Mitume.
-
53. Haitakuwa ila ukelele mmoja tu, mara wote watahudhuruishwa mbele yetu.
-
54. Basi leo nafsi yoyote haitadhulumiwa kitu, wala hamtalipwa ila yale mliyo kuwa mkiyatenda.
-
55. Hakika watu wa Peponi leo wamo shughulini, wamefurahi.
-
56. Wao na wake zao wamo katika vivuli wameegemea juu ya viti vya fakhari.
-
57. Watapata humo kila namna ya matunda na watapata kila watakacho kitaka.
-
58. "Salama!" Hiyo ndiyo kauli itokayo kwa Mola Mlezi Mwenye kurehemu.
-
59. Na enyi wakosefu! Jitengeni leo!
-
60. Je! Sikuagana nanyi, enyi wanaadamu, kuwa msimuabudu Shet`ani? Hakika yeye ni adui dhaahiri kwenu.
-
61. Na ya kwamba mniabudu Mimi? Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka.
-
62. Na bila ya shaka yeye amekwisha lipoteza kundi kubwa miongoni mwenu. Je, hamkuwa mkifikiri?
-
63. Hii basi ndiyo Jahannamu mliyo kuwa mkiahidiwa.
-
64. Ingieni leo kwa vile mlivyo kuwa mkikufuru.
-
65. Leo tunaviziba vinywa vyao, na iseme nasi mikono yao, na itoe ushahidi miguu yao kwa waliyo kuwa wakiyachuma.
-
66. Na tungeli penda tungeli yafutilia mbali macho yao, wakawa wanaiwania njia. Lakini wange ionaje?
-
67. Na tungeli taka tunge wageuza sura hapo hapo walipo, basi wasinge weza kwenda wala kurudi.
-
68. Na tunaye mzeesha tunamrudisha nyuma katika umbo. Basi je! hawazingatii?
-
69. Wala hatukumfundisha (Muhammad) mashairi, wala hayatakikani kwake hayo. Haukuwa huu ila ni ukumbusho na Qur`ani inayo bainisha.
-
70. Ili imwonye aliye hai, na neno litimie juu ya makafiri.
-
71. Je! Hawaoni kwamba tumewaumbia kutokana na iliyo fanya mikono yetu wanyama wa mifugo, na wao wakawa wenye kuwamiliki.
-
72. Na Sisi tukawadhalilishia. Basi baadhi yao wako wanao wapanda, na baadhi yao wanawala.
-
73. Na wao wanapata kwao manufaa na vinywaji. Basi je, hawashukuru?
-
74. Na wameishika miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu ili ati wapate kusaidiwa!
-
75. Hawataweza kuwasaidia. Bali hao ndio watakuwa askari wao watakao hudhurishwa.
-
76. Basi maneno yao yasikuhuzunishe. Hakika Sisi tunayajua wanayo yaweka siri na wanayo yatangaza.
-
77. Kwani mwanaadamu haoni ya kwamba Sisi tumemuumba yeye kutokana na tone la manii? Kisha sasa yeye ndio amekuwa ndiye mgomvi wa dhaahiri!
-
78. Na akatupigia mfano, na akasahau kuumbwa kwake, akasema: Ni nani huyo atakaye ihuisha mifupa nayo imekwisha mung`unyika?
-
79. Sema: Ataihuisha huyo huyo aliye iumba hapo mara ya mwanzo. Na Yeye ni Mjuzi wa kila kuumba.
-
80. Aliye kujaalieni kupata moto kutokana na mti wa kijani nanyi mkawa kwa huo mnawasha.
-
81. Kwani aliye ziumba mbingu na ardhi hawezi kuwaumba mfano wao? Kwani! Naye ndiye Muumbaji Mkuu, Mjuzi.
-
82. Hakika amri yake anapo taka kitu ni kukiambia tu: Kuwa! Na kikawa.
-
83. Basi Ametakasika yule ambaye mkononi mwake umo Ufalme wa kila kitu; na kwake Yeye mtarejeshwa.
SHIRIKI
1
Al-Fatihah
2
Al Baqara
3
Ali `Imran
4
An-Nisa
5
Al-Ma`idah
6
Al-An`am
7
Al-A`raf
8
Al-Anfal
9
At-Tawbah
10
Yunus
11
Hud
12
Yusuf
13
Ar-Ra`d
14
Ibrahim
15
Al-Hijr
16
An-Nahl
17
Al-Isra
18
Al-Kahf
19
Maryam
20
Taha
21
Al-Anbya
22
Al-Haj
23
Al-Mu`minun
24
An-Nur
25
Al-Furqan
26
Ash-Shu`ara
27
An-Naml
28
Al-Qasas
29
Al-`Ankabut
30
Ar-Rum
31
Luqman
32
As-Sajdah
33
Al-Ahzab
34
Saba
35
Faatir
36
Ya-Sin
37
As-Saffat
38
Sad
39
Az-Zumar
40
Ghafir
41
Fussilat
42
sh-Shuraa
43
Az-Zukhruf
44
Ad-Dukhan
45
Al-Jathiyah
46
Al-Ahqaf
47
Muhammad
48
Al-Fath
49
Al-Hujurat
50
Qaf
51
Adh-Dhariyat
52
At-Tur
53
An-Najm
54
Al-Qamar
55
Ar-Rahman
56
Al-Waqi`ah
57
Al-Hadid
58
Al-Mujadila
59
Al-Hashr
60
Al-Mumtahanah
61
As-Saf
62
Al-Jumu`ah
63
Al-Munafiqun
64
At-Taghabun
65
At-Talaq
66
At-Tahrim
67
Al-Mulk
68
Al-Qalam
69
Al-Haqqah
70
Al-Ma`arij
71
Nuh
72
Al-Jinn
73
Al-Muzzammil
74
Al-Muddaththir
75
Al-Qiyamah
76
Al-Insan
77
Al-Mursalat
78
An-Naba
79
An-Nazi`at
80
Abasa
81
At-Takwir
82
Al-Infitar
83
Al-Mutaffifin
84
Al-Inshiqaq
85
Al-Buruj
86
At-Tariq
87
Al-A`la
88
Al-Ghashiyah
89
Al-Fajr
90
Al-Balad
91
Ash-Shams
92
Al-Layl
93
Ad-Duhaa
94
Ash-Sharh
95
At-Tin
96
Al-`Alaq
97
Al-Qadr
98
Al-Bayyinah
99
Az-Zalzalah
100
Al-`Adiyat
101
Al-Qari`ah
102
At-Takathur
103
Al-`Asr
104
Al-Humazah
105
Al-Fil
106
Quraysh
107
Al-Ma`un
108
Al-Kawthar
109
Al-Kafirun
110
An-Nasr
111
Al-Masad
112
Al-Ikhlas
113
Al-Falaq
114
An-Nas