91. Ash-Shams - Qurani
- 1. Naapa kwa jua na mwangaza wake!
- 2. Na kwa mwezi unapo lifuatia!
- 3. Na kwa mchana unapo lidhihirisha!
- 4. Na kwa usiku unapo lifunika!
- 5. Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga!
- 6. Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza!
- 7. Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza!
- 8. Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake,
- 9. Hakika amefanikiwa aliye itakasa,
- 10. Na hakika amekhasiri aliye iviza.