As-Saffat - QURAN - Harun Yahya
-
1. Naapa kwa wanao jipanga kwa safu.
-
2. Na kwa wenye kukataza mabaya.
-
3. Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.
-
4. Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.
-
5. Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.
-
6. Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.
-
7. Na kulinda na kila shet`ani a`si.
-
8. Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.
-
9. Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.
-
10. Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng`ara.
-
11. Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata.
-
12. Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara.
-
13. Na wanapo kumbushwa hawakumbuki.
-
14. Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara.
-
15. Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri.
-
16. Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?
-
17. Hata baba zetu wa zamani?
-
18. Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.
-
19. Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona!
-
20. Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.
-
21. Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha.
-
22. Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu -
-
23. Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!
-
24. Na wasimamisheni. Hakika hao watasailiwa:
-
25. Mna nini? Mbona hamsaidiani?
-
26. Bali hii leo, watasalimu amri.
-
27. Watakabiliana wao kwa wao kuulizana.
-
28. Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia.
-
29. Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini.
-
30. Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu.
-
31. Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu.
-
32. Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.
-
33. Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja.
-
34. Hivyo ndivyo tutakavyo wafanyia wakosefu.
-
35. Wao walipo kuwa wakiambiwa La ilaha illa `Llahu Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu, wakijivuna.
-
36. Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu?
-
37. Bali huyu amekuja kwa Haki, na amewasadikisha Mitume.
-
38. Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.
-
39. Wala hamlipwi ila hayo mliyo kuwa mkiyafanya.
-
40. Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
-
41. Hao ndio watakao pata riziki maalumu,
-
42. Matunda, nao watahishimiwa.
-
43. Katika Bustani za neema.
-
44. Wako juu ya viti wamekabiliana.
-
45. Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem
-
46. Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.
-
47. Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.
-
48. Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri.
-
49. Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika.
-
50. Waingie kuulizana wenyewe kwa wenyewe.
-
51. Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa na rafiki
-
52. Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki
-
53. Ati tukisha kufa tukawa udongo na mafupa, ndio tutalipwa na kuhisabiwa?
-
54. Atasema: Je! Nyie mnawaona?
-
55. Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu.
-
56. Atasema: Wallahi! Ulikaribia kunipoteza.
-
57. Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa.
-
58. Je! Sisi hatutakufa,
-
59. Isipo kuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa.
-
60. Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa.
-
61. Kwa mfano wa haya nawatende watendao.
-
62. Je! Kukaribishwa hivi si ndio bora, au mti wa Zaqqum?
-
63. Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa walio dhulumu.
-
64. Hakika huo ni mti unao toka katikati ya Jahannamu.
-
65. Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashet`ani.
-
66. Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo.
-
67. Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji yamoto yaliyo chemka.
-
68. Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu.
-
69. Hakika waliwakuta baba zao wamepotea.
-
70. Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao.
-
71. Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani.
-
72. Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji.
-
73. Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walio onywa.
-
74. Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
-
75. Na hakika Nuhu alitwita, na Sisi ni bora wa waitikiaji.
-
76. Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa.
-
77. Na tuliwajaalia dhuriya zake ndio wenye kubakia.
-
78. Na tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja baadaye.
-
79. Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote!
-
80. Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
-
81. Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
-
82. Kisha tukawazamisha wale wengine.
-
83. Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake,
-
84. Alipo mjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima.
-
85. Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?
-
86. Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?
-
87. Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?
-
88. Kisha akapiga jicho kutazama nyota.
-
89. Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!
-
90. Nao wakamwacha, wakampa kisogo.
-
91. Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli?
-
92. Mna nini hata hamsemi?
-
93. Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia.
-
94. Basi wakamjia upesi upesi.
-
95. Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe?
-
96. Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya!
-
97. Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo!
-
98. Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini.
-
99. Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.
-
100. Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.
-
101. Basi tukambashiria mwana aliye mpole.
-
102. Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo amrishwa, utanikuta mimi, Inshallah, katika wanao subiri.
-
103. Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.
-
104. Tulimwita: Ewe Ibrahim!
-
105. Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao tenda mema.
-
106. Hakika haya ni majaribio yaliyo dhaahiri.
-
107. Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu.
-
108. Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye.
-
109. Iwe salama kwa Ibrahim!
-
110. Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
-
111. Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
-
112. Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.
-
113. Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuriya zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi.
-
114. Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni.
-
115. Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa.
-
116. Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda.
-
117. Na tukawapa wawili hao Kitabu kinacho bainisha.
-
118. Na tukawaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka.
-
119. Na tukawaachia (sifa njema) katika watu walio kuja baadaye.
-
120. Iwe salama kwa Musa na Haruni!
-
121. Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
-
122. Hakika wawili hao ni katika waja wetu walio amini.
-
123. Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume.
-
124. Alipo waambia watu wake: Hamwogopi?
-
125. Mnamwomba Baa`li na mnamwacha Mbora wa waumbaji,
-
126. Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?
-
127. Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa;
-
128. Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
-
129. Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa walio kuja baadaye.
-
130. Iwe salama kwa Ilyas.
-
131. Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
-
132. Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
-
133. Na hakika Lut`i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.
-
134. Tulipo mwokoa yeye na ahali zake wote,
-
135. Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma.
-
136. Kisha tukawaangamiza wale wengineo.
-
137. Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi,
-
138. Na usiku. Basi je! Hamyatii akilini?
-
139. Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume.
-
140. Alipo kimbia katika jahazi lilio sheheni.
-
141. Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa.
-
142. Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa.
-
143. Na ingeli kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Mwenyezi Mungu,
-
144. Bila ya shaka angeli kaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa.
-
145. Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa.
-
146. Na tukauotesha juu yake mmea wa kabila ya mung`unye.
-
147. Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi.
-
148. Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda.
-
149. Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?
-
150. Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?
-
151. Ati ni kwa uzushi wao ndio wanasema:
-
152. Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!
-
153. Ati amekhiari watoto wa kike kuliko wanaume?
-
154. Mna nini? Mnahukumu vipi nyinyi?
-
155. Hamkumbuki?
-
156. Au mnayo hoja iliyo wazi?
-
157. Basi leteni Kitabu chenu kama mnasema kweli.
-
158. Na wameweka makhusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwisha jua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa.
-
159. Subhana `Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo msingizia.
-
160. Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
-
161. Basi hakika nyinyi na mnao waabudu
-
162. Hamwezi kuwapoteza
-
163. Isipo kuwa yule atakaye ingia Motoni.
-
164. Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu.
-
165. Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu.
-
166. Na hakika sisi ndio wenye kusabihi kutakasa.
-
167. Na walikuwapo walio kuwa wakisema:
-
168. Tungeli kuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani,
-
169. Bila ya shaka tungeli kuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye ikhlasi.
-
170. Lakini waliukataa. Basi watakuja jua.
-
171. Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu walio tumwa.
-
172. Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakao nusuriwa.
-
173. Na kwamba jeshi letu ndilo litakalo shinda.
-
174. Basi waachilie mbali kwa muda.
-
175. Na watazame, nao wataona.
-
176. Je! Wanaihimiza adhabu yetu?
-
177. Basi itakapo shuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walio onywa.
-
178. Na waache kwa muda.
-
179. Na tazama, na wao wataona.
-
180. Subhana Rabbi`l`Izzat Ametakasika Mola Mlezi Mwenye enzi na yale wanayo mzulia.
-
181. Na Salamu juu ya Mitume.
-
182. Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
SHIRIKI
1
Al-Fatihah
2
Al Baqara
3
Ali `Imran
4
An-Nisa
5
Al-Ma`idah
6
Al-An`am
7
Al-A`raf
8
Al-Anfal
9
At-Tawbah
10
Yunus
11
Hud
12
Yusuf
13
Ar-Ra`d
14
Ibrahim
15
Al-Hijr
16
An-Nahl
17
Al-Isra
18
Al-Kahf
19
Maryam
20
Taha
21
Al-Anbya
22
Al-Haj
23
Al-Mu`minun
24
An-Nur
25
Al-Furqan
26
Ash-Shu`ara
27
An-Naml
28
Al-Qasas
29
Al-`Ankabut
30
Ar-Rum
31
Luqman
32
As-Sajdah
33
Al-Ahzab
34
Saba
35
Faatir
36
Ya-Sin
37
As-Saffat
38
Sad
39
Az-Zumar
40
Ghafir
41
Fussilat
42
sh-Shuraa
43
Az-Zukhruf
44
Ad-Dukhan
45
Al-Jathiyah
46
Al-Ahqaf
47
Muhammad
48
Al-Fath
49
Al-Hujurat
50
Qaf
51
Adh-Dhariyat
52
At-Tur
53
An-Najm
54
Al-Qamar
55
Ar-Rahman
56
Al-Waqi`ah
57
Al-Hadid
58
Al-Mujadila
59
Al-Hashr
60
Al-Mumtahanah
61
As-Saf
62
Al-Jumu`ah
63
Al-Munafiqun
64
At-Taghabun
65
At-Talaq
66
At-Tahrim
67
Al-Mulk
68
Al-Qalam
69
Al-Haqqah
70
Al-Ma`arij
71
Nuh
72
Al-Jinn
73
Al-Muzzammil
74
Al-Muddaththir
75
Al-Qiyamah
76
Al-Insan
77
Al-Mursalat
78
An-Naba
79
An-Nazi`at
80
Abasa
81
At-Takwir
82
Al-Infitar
83
Al-Mutaffifin
84
Al-Inshiqaq
85
Al-Buruj
86
At-Tariq
87
Al-A`la
88
Al-Ghashiyah
89
Al-Fajr
90
Al-Balad
91
Ash-Shams
92
Al-Layl
93
Ad-Duhaa
94
Ash-Sharh
95
At-Tin
96
Al-`Alaq
97
Al-Qadr
98
Al-Bayyinah
99
Az-Zalzalah
100
Al-`Adiyat
101
Al-Qari`ah
102
At-Takathur
103
Al-`Asr
104
Al-Humazah
105
Al-Fil
106
Quraysh
107
Al-Ma`un
108
Al-Kawthar
109
Al-Kafirun
110
An-Nasr
111
Al-Masad
112
Al-Ikhlas
113
Al-Falaq
114
An-Nas