At-Tur - QURAN - Harun Yahya
-
1. Naapa kwa mlima wa T`ur,
-
2. Na Kitabu kilicho andikwa
-
3. Katika ngozi iliyo kunjuliwa,
-
4. Na kwa Nyumba iliyo jengwa,
-
5. Na kwa dari iliyo nyanyuliwa,
-
6. Na kwa bahari iliyo jazwa,
-
7. Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea.
-
8. Hapana wa kuizuia.
-
9. Siku zitakapo tikisika mbingu kwa mtikiso,
-
10. Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa.
-
11. Basi ole wao siku hiyo hao wanao kadhibisha,
-
12. Ambao wanacheza katika mambo ya upuuzi.
-
13. Siku watapo sukumwa kwenye Moto kwa msukumo wa nguvu,
-
14. (Waambiwe): Huu ndio ule Moto mlio kuwa mkiukanusha!
-
15. Je! Huu ni uchawi, au hamwoni tu?
-
16. Uingieni, mkistahamili au msistahamili - ni mamoja kwenu. Hakika mnalipwa kwa mliyo kuwa mkiyatenda.
-
17. Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na neema,
-
18. Wakifurahi kwa yale aliyo wapa Mola wao Mlezi. Na Mola wao Mlezi atawalinda na adhabu ya Motoni.
-
19. Kuleni na kunyweni kwa raha kabisa kwa sababu ya mliyo kuwa mkiyatenda.
-
20. Watakuwa wameegemea juu ya viti vya enzi vilivyo pangwa kwa safu. Na tutawaoza mahuru-l-aini.
-
21. Na walio amini na dhuriya zao wakawafuata kwa Imani tutawakutanisha nao dhuriya zao, na wala hatutawapunja hata kidogo katika vitendo vyao. Kila mtu lazima atapata alicho kichuma.
-
22. Na tutawapa matunda, na nyama kama watavyo penda.
-
23. Watapeana humo bilauri zisio na vinywaji vya kuleta maneno ya upuuzi wala dhambi.
-
24. Iwe wanawapitia watumishi wao kama kwamba ni lulu zilizomo katika chaza.
-
25. Wataelekeana wakiulizana.
-
26. Waseme: Tulikuwa zamani pamoja na ahali zetu tukiogopa;
-
27. Basi Mwenyezi Mungu akatufanyia hisani na akatulinda na adhabu ya upepo wa Moto.
-
28. Hakika sisi zamani tulikuwa tukimwomba Yeye tu. Hakika Yeye ndiye Mwema Mwenye kurehemu.
-
29. Basi kumbusha! Kwani wewe, kwa neema ya Mola wako Mlezi, si kuhani wala mwendawazimu.
-
30. Au wanasema: Huyu ni mtunga mashairi, tunamtarajia kupatilizwa na dahari.
-
31. Sema: Tarajieni, na mimi pia ni pamoja nanyi katika kutarajia.
-
32. Au hizo akili zao ndio zinawaamrisha haya, au wao basi ni watu majeuri tu?
-
33. Au ndio wanasema: Ameitunga hii! Bali basi tu hawaamini!
-
34. Basi nawalete masimulizi kama haya ikiwa wao wanasema kweli.
-
35. Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?
-
36. Au wao wameziumba mbingu na ardhi? Bali hawana na yakini.
-
37. Au wanazo khazina za Mola wako Mlezi au wao ndio wenye madaraka?
-
38. Au wanazo ngazi za kusikilizia? Basi huyo msikilizaji wao na alete hoja ilio wazi!
-
39. Au Yeye Mwenyezi Mungu ana wasichana, na nyinyi ndio mna wavulana?
-
40. Au wewe unawaomba ujira, na kwa hivyo ndio wanaelemewa na uzito wa gharama?
-
41. Au wanayo ilimu ya ghaibu, nao wameandika?
-
42. Au wanataka kufanya vitimbi tu? Lakini hao walio kufuru ndio watakao tegeka.
-
43. Au wanae mungu asiye kuwa Mwenyezi Mungu? Subhanallah! Ametaksika Mwenyezi Mungu na hao wanao washirikisha naye.
-
44. Na hata wange ona pande linatoka mbinguni linaanguka wange sema: Ni mawingu yaliyo bebana.
-
45. Basi waache mpaka wakutane na siku yao watakapo hilikishwa.
-
46. Siku ambayo hila zao hazitawafaa hata kidogo, wala wao hawatanusuriwa.
-
47. Na hakika walio dhulumu watapata adhabu nyengine isiyo kuwa hii, lakini wengi wao hawajui.
-
48. Na ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi. Kwani wewe hakika uko mbele ya macho yetu, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi unapo simama,
-
49. Na usiku pia mtakase, na zinapo kuchwa nyota.
SHIRIKI
1
Al-Fatihah
2
Al Baqara
3
Ali `Imran
4
An-Nisa
5
Al-Ma`idah
6
Al-An`am
7
Al-A`raf
8
Al-Anfal
9
At-Tawbah
10
Yunus
11
Hud
12
Yusuf
13
Ar-Ra`d
14
Ibrahim
15
Al-Hijr
16
An-Nahl
17
Al-Isra
18
Al-Kahf
19
Maryam
20
Taha
21
Al-Anbya
22
Al-Haj
23
Al-Mu`minun
24
An-Nur
25
Al-Furqan
26
Ash-Shu`ara
27
An-Naml
28
Al-Qasas
29
Al-`Ankabut
30
Ar-Rum
31
Luqman
32
As-Sajdah
33
Al-Ahzab
34
Saba
35
Faatir
36
Ya-Sin
37
As-Saffat
38
Sad
39
Az-Zumar
40
Ghafir
41
Fussilat
42
sh-Shuraa
43
Az-Zukhruf
44
Ad-Dukhan
45
Al-Jathiyah
46
Al-Ahqaf
47
Muhammad
48
Al-Fath
49
Al-Hujurat
50
Qaf
51
Adh-Dhariyat
52
At-Tur
53
An-Najm
54
Al-Qamar
55
Ar-Rahman
56
Al-Waqi`ah
57
Al-Hadid
58
Al-Mujadila
59
Al-Hashr
60
Al-Mumtahanah
61
As-Saf
62
Al-Jumu`ah
63
Al-Munafiqun
64
At-Taghabun
65
At-Talaq
66
At-Tahrim
67
Al-Mulk
68
Al-Qalam
69
Al-Haqqah
70
Al-Ma`arij
71
Nuh
72
Al-Jinn
73
Al-Muzzammil
74
Al-Muddaththir
75
Al-Qiyamah
76
Al-Insan
77
Al-Mursalat
78
An-Naba
79
An-Nazi`at
80
Abasa
81
At-Takwir
82
Al-Infitar
83
Al-Mutaffifin
84
Al-Inshiqaq
85
Al-Buruj
86
At-Tariq
87
Al-A`la
88
Al-Ghashiyah
89
Al-Fajr
90
Al-Balad
91
Ash-Shams
92
Al-Layl
93
Ad-Duhaa
94
Ash-Sharh
95
At-Tin
96
Al-`Alaq
97
Al-Qadr
98
Al-Bayyinah
99
Az-Zalzalah
100
Al-`Adiyat
101
Al-Qari`ah
102
At-Takathur
103
Al-`Asr
104
Al-Humazah
105
Al-Fil
106
Quraysh
107
Al-Ma`un
108
Al-Kawthar
109
Al-Kafirun
110
An-Nasr
111
Al-Masad
112
Al-Ikhlas
113
Al-Falaq
114
An-Nas