Al-Waqi`ah - QURAN - Harun Yahya
-
1. Litakapo tukia hilo Tukio
-
2. Hapana cha kukanusha kutukia kwake.
-
3. Literemshalo linyanyualo,
-
4. Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,
-
5. Na milima itapo sagwasagwa,
-
6. Iwe mavumbi yanayo peperushwa,
-
7. Na nyinyi mtakuwa namna tatu:-
-
8. Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?
-
9. Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?
-
10. Na wa mbele watakuwa mbele.
-
11. Hao ndio watakao karibishwa
-
12. Katika Bustani zenye neema.
-
13. Fungu kubwa katika wa mwanzo,
-
14. Na wachache katika wa mwisho.
-
15. Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa.
-
16. Wakiviegemea wakielekeana.
-
17. Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele,
-
18. Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi.
-
19. Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.
-
20. Na matunda wayapendayo,
-
21. Na nyama za ndege kama wanavyo tamani.
-
22. Na Mahurulaini,
-
23. Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa.
-
24. Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
-
25. Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi,
-
26. Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama.
-
27. Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?
-
28. Katika mikunazi isiyo na miba,
-
29. Na migomba iliyo pangiliwa,
-
30. Na kivuli kilicho tanda,
-
31. Na maji yanayo miminika,
-
32. Na matunda mengi,
-
33. Hayatindikii wala hayakatazwi,
-
34. Na matandiko yaliyo nyanyuliwa.
-
35. Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya,
-
36. Na tutawafanya vijana,
-
37. Wanapendana na waume zao, hirimu moja.
-
38. Kwa ajili ya watu wa kuliani.
-
39. Fungu kubwa katika wa mwanzo,
-
40. Na fungu kubwa katika wa mwisho.
-
41. Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni?
-
42. Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka,
-
43. Na kivuli cha moshi mweusi,
-
44. Si cha kuburudisha wala kustarehesha.
-
45. Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa.
-
46. Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa,
-
47. Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa?
-
48. Au baba zetu wa zamani?
-
49. Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho
-
50. Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu.
-
51. Kisha nyinyi, mlio potea, mnao kanusha,
-
52. Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu.
-
53. Na kwa mti huo mtajaza matumbo.
-
54. Na juu yake mtakunywa maji yanayo chemka.
-
55. Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu.
-
56. Hiyo ndiyo karamu yao Siku ya Malipo.
-
57. Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki?
-
58. Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza?
-
59. Je! Mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji?
-
60. Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi
-
61. Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua.
-
62. Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki?
-
63. Je! Mnaona makulima mnayo yapanda?
-
64. Je! Ni nyinyi mnayo yaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha?
-
65. Tungeli taka tungeli yafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu,
-
66. Mkisema: Hakika sisi tumegharimika;
-
67. Bali sisi tumenyimwa.
-
68. Je! Mnayaona maji mnayo yanywa?
-
69. Je! Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha?
-
70. Tungeli penda tungeli yafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru?
-
71. Je! Mnauona moto mnao uwasha?
-
72. Ni nyinyi mlio uumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji?
-
73. Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani.
-
74. Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu.
-
75. Basi naapa kwa maanguko ya nyota,
-
76. Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua!
-
77. Hakika hii bila ya shaka ni Qur`ani Tukufu,
-
78. Katika Kitabu kilicho hifadhiwa.
-
79. Hapana akigusaye ila walio takaswa.
-
80. Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
-
81. Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza?
-
82. Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha?
-
83. Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo,
-
84. Na nyinyi wakati huo mnatazama!
-
85. Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi.
-
86. Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu,
-
87. Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli?
-
88. Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa,
-
89. Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema.
-
90. Na akiwa katika watu wa upande wa kulia,
-
91. Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia.
-
92. Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu,
-
93. Basi karamu yake ni maji yanayo chemka,
-
94. Na kutiwa Motoni.
-
95. Hakika hii ndiyo haki yenye yakini.
-
96. Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa.
SHIRIKI
1
Al-Fatihah
2
Al Baqara
3
Ali `Imran
4
An-Nisa
5
Al-Ma`idah
6
Al-An`am
7
Al-A`raf
8
Al-Anfal
9
At-Tawbah
10
Yunus
11
Hud
12
Yusuf
13
Ar-Ra`d
14
Ibrahim
15
Al-Hijr
16
An-Nahl
17
Al-Isra
18
Al-Kahf
19
Maryam
20
Taha
21
Al-Anbya
22
Al-Haj
23
Al-Mu`minun
24
An-Nur
25
Al-Furqan
26
Ash-Shu`ara
27
An-Naml
28
Al-Qasas
29
Al-`Ankabut
30
Ar-Rum
31
Luqman
32
As-Sajdah
33
Al-Ahzab
34
Saba
35
Faatir
36
Ya-Sin
37
As-Saffat
38
Sad
39
Az-Zumar
40
Ghafir
41
Fussilat
42
sh-Shuraa
43
Az-Zukhruf
44
Ad-Dukhan
45
Al-Jathiyah
46
Al-Ahqaf
47
Muhammad
48
Al-Fath
49
Al-Hujurat
50
Qaf
51
Adh-Dhariyat
52
At-Tur
53
An-Najm
54
Al-Qamar
55
Ar-Rahman
56
Al-Waqi`ah
57
Al-Hadid
58
Al-Mujadila
59
Al-Hashr
60
Al-Mumtahanah
61
As-Saf
62
Al-Jumu`ah
63
Al-Munafiqun
64
At-Taghabun
65
At-Talaq
66
At-Tahrim
67
Al-Mulk
68
Al-Qalam
69
Al-Haqqah
70
Al-Ma`arij
71
Nuh
72
Al-Jinn
73
Al-Muzzammil
74
Al-Muddaththir
75
Al-Qiyamah
76
Al-Insan
77
Al-Mursalat
78
An-Naba
79
An-Nazi`at
80
Abasa
81
At-Takwir
82
Al-Infitar
83
Al-Mutaffifin
84
Al-Inshiqaq
85
Al-Buruj
86
At-Tariq
87
Al-A`la
88
Al-Ghashiyah
89
Al-Fajr
90
Al-Balad
91
Ash-Shams
92
Al-Layl
93
Ad-Duhaa
94
Ash-Sharh
95
At-Tin
96
Al-`Alaq
97
Al-Qadr
98
Al-Bayyinah
99
Az-Zalzalah
100
Al-`Adiyat
101
Al-Qari`ah
102
At-Takathur
103
Al-`Asr
104
Al-Humazah
105
Al-Fil
106
Quraysh
107
Al-Ma`un
108
Al-Kawthar
109
Al-Kafirun
110
An-Nasr
111
Al-Masad
112
Al-Ikhlas
113
Al-Falaq
114
An-Nas