21. Al-Anbya - Qurani
- 1. IMEWAKARIBIA watu hisabu yao, nao wamo katika mghafala wanapuuza.
- 2. Hayawafikilii mawaidha mapya kutoka kwa Mola wao Mlezi ila huyasikiliza na huku wanafanya mchezo.
- 3. Zimeghafilika nyoyo zao. Na wale walio dhulumu hunong`onezana kwa siri: Ni nani ati huyu isipo kuwa ni binaadamu tu kama nyinyi! Mnauwendea uchawi hali nanyi mnaona?
- 4. Alisema: Mola wangu Mlezi anayajua yasemwayo mbinguni na katika ardhi. Na Yeye ni Mwenye kusikia Mwenye kujua.
- 5. Lakini wao walisema: Hizo ni ndoto za ovyo ovyo, bali amezizua tu, bali huyo ni mtunga mashairi. Basi atuletee miujiza kama walivyo tumwa wale wa mwanzo.
- 6. Hawakuamini kabla yao watu wa mji tulio uangamiza. Basi, je, wataamini hawa?
- 7. Na kabla yako hatukuwatuma ila watu wanaume tulio wapa wahyi (ufunuo). Basi waulizeni wenye ilimu ikiwa nyinyi hamjui.
- 8. Wala hatukuwafanya miili isiyo kula chakula, wala hawakuwa wenye kuishi milele.