logo HARUN YAHYA

Ar-Rahman - QURAN - Harun Yahya

  • 1. Arrah`man, Mwingi wa Rehema
  • 2. Amefundisha Qur`ani.
  • 3. Amemuumba mwanaadamu,
  • 4. Akamfundisha kubaini.
  • 5. Jua na mwezi huenda kwa hisabu.
  • 6. Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea.
  • 7. Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani,
  • 8. Ili msidhulumu katika mizani.
  • 9. Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani.
  • 10. Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe.
  • 11. Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba.
  • 12. Na nafaka zenye makapi, na rehani.
  • 13. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
  • 14. Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo..
  • 15. Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto.
  • 16. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
  • 17. Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili.
  • 18. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 19. Anaziendesha bahari mbili zikutane;
  • 20. Baina yao kipo kizuizi, zisiingiliane.
  • 21. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 22. Katika hizo bahari mbili zinatoka lulu na marijani.
  • 23. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 24. Na ni vyake Yeye hivi viendavyo baharini vilivyo undwa kama vilima.
  • 25. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 26. Kila kilioko juu yake kitatoweka.
  • 27. Na atabakia Mwenyewe Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.
  • 28. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 29. Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo.
  • 30. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 31. Tutakuhisabuni enyi makundi mawili.
  • 32. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 33. Enyi makundi ya majini na watu! Mkiweza kupenya kwenye mbingu na ardhi, basi penyeni! Hamtapenya ila kwa kupewa madaraka.
  • 34. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 35. Mtapelekewa muwako wa moto na shaba; wala hamtashinda.
  • 36. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 37. Itakapo pasuka mbingu ikawa nyekundu kama mafuta.
  • 38. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 39. Siku hiyo hataulizwa dhambi zake mtu wala jini.
  • 40. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 41. Watajuulikana wakosefu kwa alama zao, basi watashikwa kwa nywele zao za utosini na kwa miguu.
  • 42. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 43. Hii ndiyo Jahannamu ambayo wakosefu wakiikanusha.
  • 44. Watakuwa wakizunguka baina ya hiyo na maji ya moto yanayo chemka.
  • 45. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 46. Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi atapata Bustani mbili.
  • 47. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 48. Bustani zenye matawi yaliyo tanda.
  • 49. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 50. Ndani yake zimo chemchem mbili zinazo pita.
  • 51. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 52. Humo katika kila matunda zimo namna mbili.
  • 53. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 54. Wawe wameegemea matandiko yenye bit`ana ya hariri nzito; na matunda ya Bustani hizo yapo karibu.
  • 55. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 56. Humo watakuwamo wanawake watulizao macho yao; hajawagusa mtu kabla yao wala jini.
  • 57. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 58. Kama kwamba wao ni yakuti na marijani.
  • 59. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha.
  • 60. Ati yaweza kuwa malipo ya ihsani ila ihsani?
  • 61. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 62. Na zaidi ya hizo zipo Bustani nyengine mbili.
  • 63. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 64. Za kijani kibivu.
  • 65. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 66. Na chemchem mbili zinazo furika.
  • 67. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 68. Imo humo miti ya matunda, na mitende na mikomamanga.
  • 69. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 70. Humo wamo wanawake wema wazuri.
  • 71. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 72. Wanawake wazuri wanao tawishwa katika makhema.
  • 73. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 74. Hajawagusa mtu wala jini kabla yao.
  • 75. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 76. Wameegemea juu ya matakia ya kijani na mazulia mazuri.
  • 77. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  • 78. Limetukuka jina la Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.
SHIRIKI
Facebook
X
WhatsApp
Telegram
QR Code
QR Code