Ar-Rahman - QURAN - Harun Yahya
-
1. Arrah`man, Mwingi wa Rehema
-
2. Amefundisha Qur`ani.
-
3. Amemuumba mwanaadamu,
-
4. Akamfundisha kubaini.
-
5. Jua na mwezi huenda kwa hisabu.
-
6. Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea.
-
7. Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani,
-
8. Ili msidhulumu katika mizani.
-
9. Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani.
-
10. Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe.
-
11. Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba.
-
12. Na nafaka zenye makapi, na rehani.
-
13. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
-
14. Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo..
-
15. Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto.
-
16. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
-
17. Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili.
-
18. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
19. Anaziendesha bahari mbili zikutane;
-
20. Baina yao kipo kizuizi, zisiingiliane.
-
21. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
22. Katika hizo bahari mbili zinatoka lulu na marijani.
-
23. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
24. Na ni vyake Yeye hivi viendavyo baharini vilivyo undwa kama vilima.
-
25. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
26. Kila kilioko juu yake kitatoweka.
-
27. Na atabakia Mwenyewe Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.
-
28. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
29. Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo.
-
30. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
31. Tutakuhisabuni enyi makundi mawili.
-
32. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
33. Enyi makundi ya majini na watu! Mkiweza kupenya kwenye mbingu na ardhi, basi penyeni! Hamtapenya ila kwa kupewa madaraka.
-
34. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
35. Mtapelekewa muwako wa moto na shaba; wala hamtashinda.
-
36. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
37. Itakapo pasuka mbingu ikawa nyekundu kama mafuta.
-
38. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
39. Siku hiyo hataulizwa dhambi zake mtu wala jini.
-
40. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
41. Watajuulikana wakosefu kwa alama zao, basi watashikwa kwa nywele zao za utosini na kwa miguu.
-
42. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
43. Hii ndiyo Jahannamu ambayo wakosefu wakiikanusha.
-
44. Watakuwa wakizunguka baina ya hiyo na maji ya moto yanayo chemka.
-
45. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
46. Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi atapata Bustani mbili.
-
47. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
48. Bustani zenye matawi yaliyo tanda.
-
49. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
50. Ndani yake zimo chemchem mbili zinazo pita.
-
51. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
52. Humo katika kila matunda zimo namna mbili.
-
53. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
54. Wawe wameegemea matandiko yenye bit`ana ya hariri nzito; na matunda ya Bustani hizo yapo karibu.
-
55. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
56. Humo watakuwamo wanawake watulizao macho yao; hajawagusa mtu kabla yao wala jini.
-
57. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
58. Kama kwamba wao ni yakuti na marijani.
-
59. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha.
-
60. Ati yaweza kuwa malipo ya ihsani ila ihsani?
-
61. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
62. Na zaidi ya hizo zipo Bustani nyengine mbili.
-
63. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
64. Za kijani kibivu.
-
65. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
66. Na chemchem mbili zinazo furika.
-
67. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
68. Imo humo miti ya matunda, na mitende na mikomamanga.
-
69. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
70. Humo wamo wanawake wema wazuri.
-
71. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
72. Wanawake wazuri wanao tawishwa katika makhema.
-
73. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
74. Hajawagusa mtu wala jini kabla yao.
-
75. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
76. Wameegemea juu ya matakia ya kijani na mazulia mazuri.
-
77. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
-
78. Limetukuka jina la Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.
SHIRIKI
1
Al-Fatihah
2
Al Baqara
3
Ali `Imran
4
An-Nisa
5
Al-Ma`idah
6
Al-An`am
7
Al-A`raf
8
Al-Anfal
9
At-Tawbah
10
Yunus
11
Hud
12
Yusuf
13
Ar-Ra`d
14
Ibrahim
15
Al-Hijr
16
An-Nahl
17
Al-Isra
18
Al-Kahf
19
Maryam
20
Taha
21
Al-Anbya
22
Al-Haj
23
Al-Mu`minun
24
An-Nur
25
Al-Furqan
26
Ash-Shu`ara
27
An-Naml
28
Al-Qasas
29
Al-`Ankabut
30
Ar-Rum
31
Luqman
32
As-Sajdah
33
Al-Ahzab
34
Saba
35
Faatir
36
Ya-Sin
37
As-Saffat
38
Sad
39
Az-Zumar
40
Ghafir
41
Fussilat
42
sh-Shuraa
43
Az-Zukhruf
44
Ad-Dukhan
45
Al-Jathiyah
46
Al-Ahqaf
47
Muhammad
48
Al-Fath
49
Al-Hujurat
50
Qaf
51
Adh-Dhariyat
52
At-Tur
53
An-Najm
54
Al-Qamar
55
Ar-Rahman
56
Al-Waqi`ah
57
Al-Hadid
58
Al-Mujadila
59
Al-Hashr
60
Al-Mumtahanah
61
As-Saf
62
Al-Jumu`ah
63
Al-Munafiqun
64
At-Taghabun
65
At-Talaq
66
At-Tahrim
67
Al-Mulk
68
Al-Qalam
69
Al-Haqqah
70
Al-Ma`arij
71
Nuh
72
Al-Jinn
73
Al-Muzzammil
74
Al-Muddaththir
75
Al-Qiyamah
76
Al-Insan
77
Al-Mursalat
78
An-Naba
79
An-Nazi`at
80
Abasa
81
At-Takwir
82
Al-Infitar
83
Al-Mutaffifin
84
Al-Inshiqaq
85
Al-Buruj
86
At-Tariq
87
Al-A`la
88
Al-Ghashiyah
89
Al-Fajr
90
Al-Balad
91
Ash-Shams
92
Al-Layl
93
Ad-Duhaa
94
Ash-Sharh
95
At-Tin
96
Al-`Alaq
97
Al-Qadr
98
Al-Bayyinah
99
Az-Zalzalah
100
Al-`Adiyat
101
Al-Qari`ah
102
At-Takathur
103
Al-`Asr
104
Al-Humazah
105
Al-Fil
106
Quraysh
107
Al-Ma`un
108
Al-Kawthar
109
Al-Kafirun
110
An-Nasr
111
Al-Masad
112
Al-Ikhlas
113
Al-Falaq
114
An-Nas