90. Al-Balad - Qurani
- 1. Naapa kwa Mji huu!
- 2. Nawe unaukaa Mji huu.
- 3. Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa.
- 4. Hakika tumemuumba mtu katika taabu.
- 5. Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza?
- 6. Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.
- 7. Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?
- 8. Kwani hatukumpa macho mawili?
- 9. Na ulimi, na midomo miwili?
- 10. Na tukambainishia zote njia mbili?
- 11. Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.
- 12. Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?
- 13. Kumkomboa mtumwa;
- 14. Au kumlisha siku ya njaa
- 15. Yatima aliye jamaa,
- 16. Au masikini aliye vumbini.
- 17. Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.
- 18. Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.
- 19. Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.
- 20. Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande.