90. Al-Balad - Qurani
- 1. Naapa kwa Mji huu!
- 2. Nawe unaukaa Mji huu.
- 3. Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa.
- 4. Hakika tumemuumba mtu katika taabu.
- 5. Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza?
- 6. Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.
- 7. Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?
- 8. Kwani hatukumpa macho mawili?
- 9. Na ulimi, na midomo miwili?
- 10. Na tukambainishia zote njia mbili?