• 1. Naapa kwa Mji huu!

  • 2. Nawe unaukaa Mji huu.

  • 3. Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa.

  • 4. Hakika tumemuumba mtu katika taabu.

  • 5. Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza?

  • 6. Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.

  • 7. Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?

  • 8. Kwani hatukumpa macho mawili?

  • 9. Na ulimi, na midomo miwili?

  • 10. Na tukambainishia zote njia mbili?

  • 11. Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.

  • 12. Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?

  • 13. Kumkomboa mtumwa;

  • 14. Au kumlisha siku ya njaa

  • 15. Yatima aliye jamaa,

  • 16. Au masikini aliye vumbini.

  • 17. Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.

  • 18. Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.

  • 19. Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.

  • 20. Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande.