Al-Haqqah - QURAN - Harun Yahya
-
1. Tukio la haki.
-
2. Nini hilo Tukio la haki?
-
3. Na nini kitakujuulisha nini hilo Tukio la haki?
-
4. Thamudi na A`di waliukadhibisha Msiba unao situsha.
-
5. Basi Thamudi waliangamizwa kwa balaa kubwa mno.
-
6. Na ama A`di waliangamizwa kwa upepo mkali usio zuilika.
-
7. Alio wapelekea masiku saba, na siku nane, mfululizo bila ya kusita. Utaona watu wamepinduka kama kwamba ni magongo ya mitende yalio wazi ndani.
-
8. Basi je! Unamwona mmoja wao aliye baki?
-
9. Na Firauni na walio mtangulia, na miji iliyo pinduliwa chini juu, walileta khatia.
-
10. Wakamuasi Mtume wa Mola wao Mlezi, ndipo Yeye Mola akawakamata kwa mkamato ulio zidi nguvu.
-
11. Maji yalipo furika Sisi tulikupandisheni katika safina,
-
12. Ili tuyafanye hayo kuwa ni waadhi kwenu na kila sikio linalo sikia liyahifadhi.
-
13. Na litapo pulizwa barugumu mpulizo mmoja tu,
-
14. Na ardhi na milima ikaondolewa, na ikavunjwa kwa mvunjo mmoja,
-
15. Siku hiyo ndio Tukio litatukia.
-
16. Na mbingu zitapasuka, kwani siku hiyo zitakuwa dhaifu kabisa.
-
17. Na Malaika watakuwa pembezoni mwa mbingu; na wanane juu ya hawa watakuwa wamebeba Kiti cha Enzi cha Mola wako Mlezi.
-
18. Siku hiyo mtahudhurishwa - haitafichika siri yoyote yenu.
-
19. Basi ama atakaye pewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, atasema: Haya someni kitabu changu!
-
20. Hakika nalijua ya kuwa nitapokea hisabu yangu.
-
21. Basi yeye atakuwa katika maisha ya kupendeza,
-
22. Katika Bustani ya juu,
-
23. Matunda yake yakaribu.
-
24. Waambiwe: Kuleni na mnywe kwa furaha kwa sababu ya mlivyo tanguliza katika siku zilizo pita.
-
25. Na ama atakaye pewa kitabu chake katika mkono wake wa kushoto, basi yeye atasema: Laiti nisingeli pewa kitabu changu!
-
26. Wala nisingeli jua nini hisabu yangu.
-
27. Laiti mauti ndiyo yangeli kuwa ya kunimaliza kabisa.
-
28. Mali yangu hayakunifaa kitu.
-
29. Madaraka yangu yamenipotea.
-
30. (Pasemwe): Mshikeni! Mtieni pingu!
-
31. Kisha mtupeni Motoni!
-
32. Tena mtatizeni katika mnyororo wenye urefu wa dhiraa sabiini!
-
33. Kwani huyo hakika alikuwa hamuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu,
-
34. Wala hahimizi kulisha masikini.
-
35. Basi leo hapa hana jamaa wa kumwonea uchungu,
-
36. Wala hana chakula ila usaha wa watu wa Motoni.
-
37. Chakula hicho hawakili ila wakosefu.
-
38. Basi naapa kwa mnavyo viona,
-
39. Na msivyo viona,
-
40. Kwa hakika hii ni kauli iliyo letwa na Mjumbe mwenye hishima.
-
41. Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana mnayo yaamini.
-
42. Wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayo yakumbuka.
-
43. Ni uteremsho utokao kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
-
44. Na lau kama angeli tuzulia baadhi ya maneno tu,
-
45. Bila ya shaka tungeli mshika kwa mkono wa kulia,
-
46. Kisha kwa hakika tungeli mkata mshipa mkubwa wa moyo!
-
47. Na hapana yeyote katika nyinyi ambaye angeli weza kutuzuia.
-
48. Kwa hakika hii ni mawaidha kwa wachamngu.
-
49. Na hakika Sisi bila ya shaka tunajua kwamba miongoni mwenu wapo wanao kadhibisha.
-
50. Na hakika bila ya shaka itakuwa ni majuto kwa wanao kataa.
-
51. Na hakika hii bila ya shaka ni haki ya yakini.
-
52. Basi litakase jina la Mola wako Mlezi Mtukufu.
SHIRIKI
1
Al-Fatihah
2
Al Baqara
3
Ali `Imran
4
An-Nisa
5
Al-Ma`idah
6
Al-An`am
7
Al-A`raf
8
Al-Anfal
9
At-Tawbah
10
Yunus
11
Hud
12
Yusuf
13
Ar-Ra`d
14
Ibrahim
15
Al-Hijr
16
An-Nahl
17
Al-Isra
18
Al-Kahf
19
Maryam
20
Taha
21
Al-Anbya
22
Al-Haj
23
Al-Mu`minun
24
An-Nur
25
Al-Furqan
26
Ash-Shu`ara
27
An-Naml
28
Al-Qasas
29
Al-`Ankabut
30
Ar-Rum
31
Luqman
32
As-Sajdah
33
Al-Ahzab
34
Saba
35
Faatir
36
Ya-Sin
37
As-Saffat
38
Sad
39
Az-Zumar
40
Ghafir
41
Fussilat
42
sh-Shuraa
43
Az-Zukhruf
44
Ad-Dukhan
45
Al-Jathiyah
46
Al-Ahqaf
47
Muhammad
48
Al-Fath
49
Al-Hujurat
50
Qaf
51
Adh-Dhariyat
52
At-Tur
53
An-Najm
54
Al-Qamar
55
Ar-Rahman
56
Al-Waqi`ah
57
Al-Hadid
58
Al-Mujadila
59
Al-Hashr
60
Al-Mumtahanah
61
As-Saf
62
Al-Jumu`ah
63
Al-Munafiqun
64
At-Taghabun
65
At-Talaq
66
At-Tahrim
67
Al-Mulk
68
Al-Qalam
69
Al-Haqqah
70
Al-Ma`arij
71
Nuh
72
Al-Jinn
73
Al-Muzzammil
74
Al-Muddaththir
75
Al-Qiyamah
76
Al-Insan
77
Al-Mursalat
78
An-Naba
79
An-Nazi`at
80
Abasa
81
At-Takwir
82
Al-Infitar
83
Al-Mutaffifin
84
Al-Inshiqaq
85
Al-Buruj
86
At-Tariq
87
Al-A`la
88
Al-Ghashiyah
89
Al-Fajr
90
Al-Balad
91
Ash-Shams
92
Al-Layl
93
Ad-Duhaa
94
Ash-Sharh
95
At-Tin
96
Al-`Alaq
97
Al-Qadr
98
Al-Bayyinah
99
Az-Zalzalah
100
Al-`Adiyat
101
Al-Qari`ah
102
At-Takathur
103
Al-`Asr
104
Al-Humazah
105
Al-Fil
106
Quraysh
107
Al-Ma`un
108
Al-Kawthar
109
Al-Kafirun
110
An-Nasr
111
Al-Masad
112
Al-Ikhlas
113
Al-Falaq
114
An-Nas