An-Naba - QURAN - Harun Yahya
-
1. WANAULIZANA nini?
-
2. Ile khabari kuu,
-
3. Ambayo kwayo wanakhitalifiana.
-
4. La! Karibu watakuja jua.
-
5. Tena la! Karibu watakuja jua.
-
6. Kwani hatukuifanya ardhi kama tandiko?
-
7. Na milima kama vigingi?
-
8. Na tukakuumbeni kwa jozi?
-
9. Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko?
-
10. Na tukaufanya usiku ni nguo?
-
11. Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia maisha?
-
12. Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu?
-
13. Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto;
-
14. Na tukateremsha maji yanayo anguka kwa kasi kutoka mawinguni,
-
15. Ili tutoe kwayo nafaka na mimea,
-
16. Na mabustani yenye miti iliyo kamatana.
-
17. Hakika siku ya uamuzi imewekewa wakati wake,
-
18. Siku litapo pulizwa barugumu, nanyi mtakuja kwa makundi,
-
19. Na mbingu zitafunguliwa, ziwe milango,
-
20. Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi.
-
21. Hakika Jahannamu inangojea!
-
22. Kwa walio asi ndio makaazi yao,
-
23. Wakae humo karne baada ya karne,
-
24. Hawataonja humo chochote kibaridi wala kinywaji,
-
25. Ila maji yamoto sana na usaha,
-
26. Ndio jaza muwafaka.
-
27. Hakika hao hawakuwa wakitaraji kuwa kuna hisabu.
-
28. Na wakikanusha Aya zetu kwa nguvu.
-
29. Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika.
-
30. Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu!
-
31. Hakika wachamngu wanastahiki kufuzu,
-
32. Mabustani na mizabibu,
-
33. Na wake walio lingana nao,
-
34. Na bilauri zilizo jaa,
-
35. Hawatasikia humo upuuzi wala uwongo -
-
36. Malipo kutoka kwa Mola wako Mlezi, kipawa cha kutosha.
-
37. Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, Arrahman, Mwingi wa rehema; hawamiliki usemi mbele yake!
-
38. Siku atakapo simama Roho na Malaika kwa safu. Hawatasema ila Mwingi wa rehema aliye mruhusu, na atasema yaliyo sawa tu.
-
39. Hiyo ndiyo Siku ya haki. Basi anaye taka na ashike njia arejee kwa Mola wake Mlezi.
-
40. Hakika tumekuhadharisheni adhabu iliyo karibu kufika; Siku ambayo mtu atakapo ona yaliyo tangulizwa na mikono yake; na kafiri atasema: Laiti ningeli kuwa udongo!
SHIRIKI
1
Al-Fatihah
2
Al Baqara
3
Ali `Imran
4
An-Nisa
5
Al-Ma`idah
6
Al-An`am
7
Al-A`raf
8
Al-Anfal
9
At-Tawbah
10
Yunus
11
Hud
12
Yusuf
13
Ar-Ra`d
14
Ibrahim
15
Al-Hijr
16
An-Nahl
17
Al-Isra
18
Al-Kahf
19
Maryam
20
Taha
21
Al-Anbya
22
Al-Haj
23
Al-Mu`minun
24
An-Nur
25
Al-Furqan
26
Ash-Shu`ara
27
An-Naml
28
Al-Qasas
29
Al-`Ankabut
30
Ar-Rum
31
Luqman
32
As-Sajdah
33
Al-Ahzab
34
Saba
35
Faatir
36
Ya-Sin
37
As-Saffat
38
Sad
39
Az-Zumar
40
Ghafir
41
Fussilat
42
sh-Shuraa
43
Az-Zukhruf
44
Ad-Dukhan
45
Al-Jathiyah
46
Al-Ahqaf
47
Muhammad
48
Al-Fath
49
Al-Hujurat
50
Qaf
51
Adh-Dhariyat
52
At-Tur
53
An-Najm
54
Al-Qamar
55
Ar-Rahman
56
Al-Waqi`ah
57
Al-Hadid
58
Al-Mujadila
59
Al-Hashr
60
Al-Mumtahanah
61
As-Saf
62
Al-Jumu`ah
63
Al-Munafiqun
64
At-Taghabun
65
At-Talaq
66
At-Tahrim
67
Al-Mulk
68
Al-Qalam
69
Al-Haqqah
70
Al-Ma`arij
71
Nuh
72
Al-Jinn
73
Al-Muzzammil
74
Al-Muddaththir
75
Al-Qiyamah
76
Al-Insan
77
Al-Mursalat
78
An-Naba
79
An-Nazi`at
80
Abasa
81
At-Takwir
82
Al-Infitar
83
Al-Mutaffifin
84
Al-Inshiqaq
85
Al-Buruj
86
At-Tariq
87
Al-A`la
88
Al-Ghashiyah
89
Al-Fajr
90
Al-Balad
91
Ash-Shams
92
Al-Layl
93
Ad-Duhaa
94
Ash-Sharh
95
At-Tin
96
Al-`Alaq
97
Al-Qadr
98
Al-Bayyinah
99
Az-Zalzalah
100
Al-`Adiyat
101
Al-Qari`ah
102
At-Takathur
103
Al-`Asr
104
Al-Humazah
105
Al-Fil
106
Quraysh
107
Al-Ma`un
108
Al-Kawthar
109
Al-Kafirun
110
An-Nasr
111
Al-Masad
112
Al-Ikhlas
113
Al-Falaq
114
An-Nas