27. Hakika hao hawakuwa wakitaraji kuwa kuna hisabu.
28. Na wakikanusha Aya zetu kwa nguvu.
29. Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika.
30. Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu!
31. Hakika wachamngu wanastahiki kufuzu,
32. Mabustani na mizabibu,
33. Na wake walio lingana nao,
34. Na bilauri zilizo jaa,
35. Hawatasikia humo upuuzi wala uwongo -
36. Malipo kutoka kwa Mola wako Mlezi, kipawa cha kutosha.
37. Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, Arrahman, Mwingi wa rehema; hawamiliki usemi mbele yake!
38. Siku atakapo simama Roho na Malaika kwa safu. Hawatasema ila Mwingi wa rehema aliye mruhusu, na atasema yaliyo sawa tu.
39. Hiyo ndiyo Siku ya haki. Basi anaye taka na ashike njia arejee kwa Mola wake Mlezi.
40. Hakika tumekuhadharisheni adhabu iliyo karibu kufika; Siku ambayo mtu atakapo ona yaliyo tangulizwa na mikono yake; na kafiri atasema: Laiti ningeli kuwa udongo!