Al-Mursalat - QURAN - Harun Yahya
-
1. Naapa kwa zinazo tumwa kwa upole!
-
2. Na zinazo vuma kwa kasi!
-
3. Na zikaeneza maeneo yote!
-
4. Na zinazo farikisha zikatawanya!
-
5. Na zinazo peleka mawaidha!
-
6. Kwa kuudhuru au kuonya,
-
7. Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka yatakuwa!
-
8. Wakati nyota zitakapo futwa,
-
9. Na mbingu zitakapo pasuliwa,
-
10. Na milima itakapo peperushwa,
-
11. Na Mitume watakapo wekewa wakati wao,
-
12. Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo?
-
13. Kwa siku ya kupambanua!
-
14. Na nini kitakacho kujuulisha siku ya kupambanua ni nini?
-
15. Ole wao, siku hiyo hao wanao kanusha!
-
16. Kwani hatukuwaangamiza walio tangulia?
-
17. Kisha tukawafuatilizia walio fuatia?
-
18. Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu!
-
19. Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
-
20. Kwani hatukukuumbeni kwa maji ya kudharauliwa?
-
21. Kisha tukayaweka mahali pa utulivu madhubuti?
-
22. Mpaka muda maalumu?
-
23. Tukakadiria na Sisi ni wabora wa kukadiria.
-
24. Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
-
25. Kwani hatukuifanya ardhi yenye kukusanya
-
26. Walio hai na maiti?
-
27. Na ndani yake tukaweka milima mirefu yenye kuthibiti, na tunakunywesheni maji matamu?
-
28. Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
-
29. Nendeni kwenye adhabu mliyo kuwa mkiikanusha!
-
30. Nendeni kwenye kivuli chenye mapande matatu!
-
31. Hakikingi moto, wala hakiwaepushi na mwako.
-
32. Hakika Moto huo unatoa macheche kama majumba!
-
33. Kama kwamba ni ngamia wa rangi ya manjano!
-
34. Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
-
35. Hii ni siku ambayo hawatatamka kitu,
-
36. Wala hawataruhusiwa kutoa udhuru.
-
37. Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!
-
38. Hii ndiyo siku ya kupambanua. Tumekukusanyeni nyinyi na walio tangulia.
-
39. Ikiwa mnayo hila, nifanyieni hila Mimi!
-
40. Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!
-
41. Hakika wachamngu watakuwa katika vivuli na chemchem,
-
42. Na matunda wanayo yapenda,
-
43. Kuleni na kunyweni kwa furaha kwa yale mliyo kuwa mkiyatenda.
-
44. Hakika ndio kama hivyo tunavyo walipa watendao mema.
-
45. Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
-
46. Kuleni na mjifurahishe kidogo tu. Hakika nyinyi ni wakosefu!
-
47. Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
-
48. Na wakiambiwa: Inameni! Hawainami.
-
49. Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
-
50. Basi maneno gani baada ya haya watayaamini?
SHIRIKI
1
Al-Fatihah
2
Al Baqara
3
Ali `Imran
4
An-Nisa
5
Al-Ma`idah
6
Al-An`am
7
Al-A`raf
8
Al-Anfal
9
At-Tawbah
10
Yunus
11
Hud
12
Yusuf
13
Ar-Ra`d
14
Ibrahim
15
Al-Hijr
16
An-Nahl
17
Al-Isra
18
Al-Kahf
19
Maryam
20
Taha
21
Al-Anbya
22
Al-Haj
23
Al-Mu`minun
24
An-Nur
25
Al-Furqan
26
Ash-Shu`ara
27
An-Naml
28
Al-Qasas
29
Al-`Ankabut
30
Ar-Rum
31
Luqman
32
As-Sajdah
33
Al-Ahzab
34
Saba
35
Faatir
36
Ya-Sin
37
As-Saffat
38
Sad
39
Az-Zumar
40
Ghafir
41
Fussilat
42
sh-Shuraa
43
Az-Zukhruf
44
Ad-Dukhan
45
Al-Jathiyah
46
Al-Ahqaf
47
Muhammad
48
Al-Fath
49
Al-Hujurat
50
Qaf
51
Adh-Dhariyat
52
At-Tur
53
An-Najm
54
Al-Qamar
55
Ar-Rahman
56
Al-Waqi`ah
57
Al-Hadid
58
Al-Mujadila
59
Al-Hashr
60
Al-Mumtahanah
61
As-Saf
62
Al-Jumu`ah
63
Al-Munafiqun
64
At-Taghabun
65
At-Talaq
66
At-Tahrim
67
Al-Mulk
68
Al-Qalam
69
Al-Haqqah
70
Al-Ma`arij
71
Nuh
72
Al-Jinn
73
Al-Muzzammil
74
Al-Muddaththir
75
Al-Qiyamah
76
Al-Insan
77
Al-Mursalat
78
An-Naba
79
An-Nazi`at
80
Abasa
81
At-Takwir
82
Al-Infitar
83
Al-Mutaffifin
84
Al-Inshiqaq
85
Al-Buruj
86
At-Tariq
87
Al-A`la
88
Al-Ghashiyah
89
Al-Fajr
90
Al-Balad
91
Ash-Shams
92
Al-Layl
93
Ad-Duhaa
94
Ash-Sharh
95
At-Tin
96
Al-`Alaq
97
Al-Qadr
98
Al-Bayyinah
99
Az-Zalzalah
100
Al-`Adiyat
101
Al-Qari`ah
102
At-Takathur
103
Al-`Asr
104
Al-Humazah
105
Al-Fil
106
Quraysh
107
Al-Ma`un
108
Al-Kawthar
109
Al-Kafirun
110
An-Nasr
111
Al-Masad
112
Al-Ikhlas
113
Al-Falaq
114
An-Nas