101. Al-Qari`ah - Qurani
- 1. Inayo gonga!
- 2. Nini Inayo gonga?
- 3. Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga?
- 4. Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika;
- 5. Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa!
- 6. Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito,
- 7. Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza.
- 8. Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu,
- 9. Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya!
- 10. Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo?
- 11. Ni Moto mkali!