85. Al-Buruj - Qurani
- 1. Naapa kwa mbingu yenye Buruji!
- 2. Na kwa siku iliyo ahidiwa!
- 3. Na kwa shahidi na kinacho shuhudiwa!
- 4. Wameangamizwa watu wa makhandaki
- 5. Yenye moto wenye kuni nyingi,
- 6. Walipo kuwa wamekaa hapo,
- 7. Na wao ni mashahidi wa yale waliyo kuwa wakiwafanyia Waumini.
- 8. Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa wakimuamini Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Msifiwa,
- 9. Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Mwenyezi Mungu ni shaahidi wa kila kitu.